Thursday, May 14, 2015

MAPATO YA NDANI YAIMARISHWE KUFANIKISHA MALENGO YA MILLENIA

IMG_7724
Pichani juu na chini ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano Wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy akiwasilisha mada jinsi mataifa yalivyofikia SDGs, michakato inayoendelea na namna ambavyo Tanzania inaweza kunufaika na mkakati mzima wa maendeleo.
Na  Mwandishi Wetu
 MKURUGENZI wa Kupunguza Umasikini kutoka Wizara ya Fedha,  Anna Mwasha amesema changamoto za uwezo wa kifedha kutekeleza miradi mbalimbali iliyokuwa katika Malengo ya Milennia, zinatoa ishara tosha ya kubadili mikakati ili kuwa na mafanikio katika Mipango ijayo ya Maendeleo Endelevu (SDGs)
Alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na washiriki wa kongamano,  linalojadili yaliyojiri katika Malengo ya Millenia na nini kinastahili kufanywa katika SDGs ili kuhakikisha mafanikio.
 Alisema ipo haja ya kuimarisha makusanyo ya fedha  za ndani na kuacha kutegemea wahisani, kwa kuwa moja ya sababu za kushindwa kutekelezwa kwa Malengo ya Millenia ni ahadi za wahisani kutotekelezwa.
Alisema kipengele cha nane katika Malengo ya Millennia, kiligusia ushirikiano wa kimataifa, ahadi ambazo amesema ukiachia nchi za Luxemburg, Denmark, Sweden na Norway, mataifa mengi hayakutoa asilimia 0.7 ya pato lao la ndani, ambalo lilikubalika kimataifa kusaidia Malengo ya Millennia kwa nchi masikini.
Alisema ili kuwepo na mafanikio katika miradi mipya na ile inayoendelezwa kutoka MDGs,  iko haja ya kuangalia jamii iliyopo vijijini,  ambako ndiko kwenye umasikini wa kutisha, ingawa Tanzania imefanya vyema kuondokana na umasikini wa chakula.
Umasikini wa chakula umepungua hadi asilimia 9 wakati Malengo ya Millenia yalikuwa ni asilimia 11.
Alisema ipo haja ya kufungua mawasiliano ya vijijini, kuinua kilimo, kuwapatia nafasi ya masoko na kuinua huduma za jamii.
Pamoja na kuzungumzia uwezo wa kifedha, alisisitiza haja ya wadau kuangalia namna ya kushirikisha sekta binafsi katika kutafuta vyanzo vya fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ili kukabili umasikini.
Alisema mahitaji ya msingi katika kupunguza umasikini, hayajafikiwa kwani tumefikia asilimia 28.2 wakati tulitakiwa kuwa asilimia 19.
Alisema ipo haja kubwa ya kuangalia utekelezaji wa malengo endelevu kwa kuoanisha na mikakati mingine ya kidunia na ya kikanda, huku kazi kubwa ikiwa kuhakikisha malengo yote 17 yanatekelezwa katika muda uliopangwa.
 Katika kongamano hilo, washiriki walipata nafasi ya kumsikia Balozi Celestine Mushy kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, akichambua jinsi mataifa yalivyofikia SDGs, michakato inayoendelea na namna ambavyo anafikiri Tanzania inaweza kunufaika na mkakati mzima wa maendeleo.
Pia katika majadiliano, washiriki waliozungumzia haja ya kuangalia takwimu kwa kuoanisha kwani zimekuwa zikitafutwa na kila mtu mpaka hazijulikani nani yuko sahihi.
Aidha, walitaka mkakati wa kiviwanda ndio uzingatiwe kwani ndio unaoonesha dira ya kufanikisha maendeleo ya kitaifa, kikanda na kibara.
Kongamano hilo liliendeshwa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Uchumi (ESRF) kwa ufadhili wa UNDP.
IMG_7701
Sehemu ya washiriki wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa kwenye kongamano hilo.
IMG_7792
Pichani juu na chini baadhi ya wadau walioshiriki kwenye kongamano hilo wakichangia mada kwenye kongamano hilo.
IMG_7692
Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)- Programme, Amon Manyama akizungumza kwenye kongamano la siku moja linalojadili yaliyojiri katika Malengo ya Millenia na nini kinastahili kufanywa katika SDG's ili kuhakikisha mafanikio lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Uchumi na Utafiti wa Kijamii nchini (ESRF).
IMG_7697
Mkurugenzi wa kupunguza  umaskini kutoka Wizara ya Fedha, Ana Mwasha (kulia) akifungua kongamano,  linalojadili yaliyojiri katika Malengo ya Millenia na nini kinastahili kufanywa katika SDG's ili kuhakikisha mafanikio katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Uchumi na Utafiti wa Kijamii nchini (ESRF). Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi  wa Taasisi ya Uchumi na Utafiti wa Kijamii nchini (ESRF) Dk.Oswald Mashindano na Katikati ni Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)- Programme, Amon Manyama.

Monday, March 9, 2015

TAMASHA LA VYAKULA VYA ASILI LILIVYOFANA UMBRELLA GARDEN SIKU YA WANAWAKE

        ·       wafanyabiashara watakiwa kuanzisha kituo cha utalii wa chakula cha asili

Na Seif Mangwangi, Tanzaniasasablog

WAFANYABIASHARA  wametakiwa kubuni mbinu mpya ya kutangaza sekta ya utalii nchini kwa kuanzisha vituo cha utalii wa vyakula vya asili ili kuvutia watalii wanaotembelea jiji la Arusha kujionea vyakula hivyo na hatimaye kupata mlo kamili wenye asili ya makabila ya Tanzania.
Mratibu wa Sensa mkoa wa Arusha Bi.Magreth Martin akizungumza na wadau
pamoja na wakazi wa jiji la Arusha waliofika kwenye tamasha hilo

Rai hiyo inetolewa jana jijini hapa na Mratibu wa takwimu Mkoa wa Arusha, Magreth Martin katika hotuba yake wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani iliyoazimishwa sambamba na tamasha la chakula cha asili cha kiafrika (African food festival) chini ya uongozi wa mgahawa wa umbrella.


Alisema Tanzania imebarikiwa kuwa na aina mbalimbali za utalii ambazo zimekuwa zikivutia wageni wa ndani na wengine kutoka nje ya nchi lakini hakuna kituo cha utalii wa vyakula vya asili ambapo wageni mbalimbali wanaweza kutembelea na kupata chakula.
Magreth alisema tamasha la chakula cha kiasili lililoandaliwa na uongozi wa Umbrella ni mfano mzuri wa kuigwa na kutoa wito kwa uongozi huo kuangalia namna ya kuanzisha kituo rasmi cha mapishi ya asili ili kuvutia wageni wa ndani na nje ya nchi wanaotembelea jiji la Arusha kwa shughuli mbalimbali.
Meneja wa Saccos katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Christine Julius
akizunguka katika tamasha hilo 
“ Watanzania tumebarikiwa kuwa na vivutio vingi sana vya utalii, lakini hatujaweza kuvitumia ipasavyo, ninachowaomba watanzania wenzangu, embu angalieni namna bora ya kuanzisha kituo cha utalii wa vyakula vya kiasili ili wageni wanaokuja Arusha na watalii kutoka nje ya nchi waweze kujua makabila yetu kwa njia ya vyakula lakini pia waweze kupata mlo mzuri kupitia vyakula hivyo,”alisema.
Alisema tunapoazimisha siku ya wanawake duniani lazima tuangalie na namna ya kuwakumbuka na kutambua umuhimu wao na kwamba maadhimisho hayo yaliyoenda sanjari na chakula cha asili ni siku muhimu sana kwa kina mama.
“Naamini siku ya leo ni muhimu sana,  lakini isiishie tu kufanya tamasha hili, itapendeza kama mtaanzisha kituo cha utalii wa chakula cha asili ili wageni mbalimbali wanapokuja arusha waweze kupata chakula halisi na kujionea utamaduni wa mtanzania, hata kama ni nyie umbrella fanyeni, hii itawajengea heshima sana,”alisema Magreth.
Mkurugenzi wa mgahawa wa Umbrella, Elihuruma Msengi alisema huwezi kumkumbuka Mwanamke kama hutotambua majukumu yake katika jamii ikiwemo utayarishaji wa chakula cha asili ili kuhakikisha afya ya familia yake inakuwa bora na imara.
Alisema wameamua kuanzisha tamasha hilo la chakula cha asili kwa lengo la kuonyesha umuhimu wa vyakula hivyo kwa afya ya binaadam na kuhamasisha jamii kuacha kutumia vyakula vyenye kemikali ambavyo vimekuwa vikielezwa kuchangia maradhi mengi katika afya ya binaadam.
“Uongozi wa Umbrella umepanga kufanya tamasha hili mara kwa mara ili kuwahamasisha  watanzania matumizi ya vyakula vya asili lakini pia tunachukua mawazo ya Mama yetu kuona namna ya kuanzisha kituo cha utalii wa vyakula vya asili ili na wageni wanaotembelea nchini waweze kuona asili yetu katika chakula,”alisema.
Katika tamasha hilo lililovutia wakazi wengi wa jiji la Arusha, watu walipata nafasi ya kula vyakula mbalimbali vya asili kama vile mlenda kwa makabila ya kanda ya kati na pwani, loshoro inayoliwa na wamaasai, matoke, kisamvu, supu ya pweza,  bada, maghimbi, maboga, mihogo,viazi, .  


wakazi wa Jiji la Arusha waliofika wakichukua chakula

Wakazi wa Jiji la Arusha wakimsikilia mgeni rasmi Meneja wa Saccos ya Mkoa wa Arusha katika tamasha la chakula cha asili ya kiafrika katika mgahawa wa Umbrella

wakazi wa Arusha waliofika kwenye tamasha la Africa Food Festival wakiteta

mgeni rasmi katika Tamasha hilo Christine Julius akizungumza na wageni walifika katika tamasha hilo

mfanyakazi wa kituo cha radio 5 cha jijini Arusha, Ashura Mohamed akipata chakula cha asili, mkononi akiwa kashikilia mlenda

wadau wakipata chakula

mtoto akishangaa chakula aina ya makande kinacholiwa na kabila la wapare 

mmoja wa wageni akipakuliwa mboga aina ya kisamvu

mboga za aina mbalimbali kama hapa inavyoonekana ni dagaa waliopikwa kwa ustadi wa hali ya juu

wakazi wa jiji la Arusha wakipakuliwa chakula cha aina mbalimbali

mmoja ya wakazi wa jiji la Arusha ambae jina lake halikuweza kupatikana mara moja akipakua mchuzi wa pweza

wafanyakazi wa kituo cha radio5 wakisubiri kupakua chakula 

Nyama choma pia ilikuwa ikipatikana katika tamasha hilo

waandishi wa habari wakizungumza na uongozi wa mgahawa wa umbrella

wasanii aika na nareel wakitumbuiza jukwaani katika tamasha hilo 
mkurugenzi wa umbrella garden, Elihuruma Msengi akizungumza kukaribisha wageni katika tamasha hilo 



wakazi wa arusha pia walipa fursa ya kuona nguo za asili katika tamasha hilo 


wadau wakiwa katika viwanja vya umbrella

EAC CELEBRATES INTERNATIONAL WOMEN’S DAY




East African Community

PRESS RELEASE

EAC CELEBRATES INTERNATIONAL WOMEN’S DAY

The Arusha City Council, Women Organisations, Staff members of the EAC and other invited guests partaking in a ‘Walk for Gender Equality’ around designated areas in Arusha town during EAC’s International Women’s Day celebrations. 
..EAC Secretariat raises awareness on women’s rights and gender equality during International Women’s Day celebrations.
 The EAC Secretariat celebrated International Women’s Day as part of its strategy to increase the participation of women in the EAC’s regional integration process. Under this year’s theme ‘Make it Happen,’ the Deputy Secretary General, together with the Arusha City Council, Women Organisations, Staff members of the EAC and other invited guests, took part in a ‘Walk for Gender Equality’ around designated areas in Arusha town, visited the Maternity Unit of Mt. Meru Regional Hospital, launched the EAC International Women’s website, and benefitted from various presentations and key note addresses on women’s rights and gender equality.

“International Women’s Day is a time to reflect on the achievements that women in the EAC have attained in the last 20 years, as well as to identify the challenges that still impede their full potential,” said Hon. Jesca Eriyo, EAC’s Deputy Secretary General, Productive and Social Sectors.

“We recognise that women make a significant contribution towards the process of economic transformation and sustainable growth, and that is why we want to emphasise the importance of their effective participation, empowerment and development in EAC’s integration process,” she said.  

‘Make it Happen’ stands as a global call for women and men to concretize Gender Equality, which is a follow up to the prepositions from the 20th Anniversary of the Fourth World Conference on Women held in Beijing in 1995.

Gender equality can only be attained when women and men enjoy the same rights and opportunities across all sectors of society, including economic participation and decision-making, and when the different behaviours, aspirations and needs of women and men are equally valued and favoured.

On average women are paid lower salaries than men for the same work. Women also continue to be victims of violence, with rape and domestic violence listed as significant causes of disability and death among women worldwide.

As a way of fulfilling their commitment to an East African Community where women are able to participate as equal partners, decision makers, and beneficiaries of the sustainable development of their societies, the EAC has created a Sectoral Council on Gender to handle gender issues by proposing legal and policy frameworks accordingly.

To this end, this would make meaningful and sustainable changes for women and girls.

EAC’s Deputy Secretary General, Productive and Social Sectors, Hon. Jesca Eriyo (second right) and Mr. Bernd Malthup Head of EAC/GIZ Programme, Arusha (far left), donating hospital equipments to the Maternity Unit of Mt. Meru Regional Hospital in Arusha. 

EAC’s Deputy Secretary General, Productive and Social Sectors, Hon. Jesca Eriyo (first left) and Head of EAC/GIZ Programme, Arusha (second left), held a special tree planting event at the EAC Headquarters in Arusha to mark International Women’s Day. 

EAC’s Deputy Secretary General, Productive and Social Sectors, Hon. Jesca Eriyo (centre right) and Mr. Bernd Malthup Head of EAC/GIZ Programme, Arusha (centre left) sitting in for a group photo with designated guests and EAC Staff members who are attending EAC International Women’s Day celebrations





Saturday, March 7, 2015

WAKAZI 10000 KUNUFAIKA NA UKARABATI BWAWA LA KALEMAWE

DSC_0082
Pichani juu na chini ni washiriki wa kongamano hilo la siku moja ambao ni madiwani wa kata za Same, mainjinia  na wakandarasi kutoka halmashauri ya wilaya ya Same pamoja na wataalam kutoka UNDCF.
20140626_124641
Pichani juu na chini ni muonekano wa bwawa la Kalemawe lililopo wilayani Same mkoani Kilimanjaro wakati UNCDF walipotembelea eneo hilo.
DSC_0072
Mkuu wa wilaya ya Same, Herman Kapufi akisisitiza jambo kwenye kongamano hilo lililowakutanisha madiwani wa kata za halmshauri ya wilaya ya Same na wataalam kutoka UNCDF kujadili pamoja kabla ya utekelezaji.
DSC_0067
Mkuu wa wilaya ya Same, Herman Kapufi akizungumza kwenye kongamano la siku moja lililofanyika jijini Dar kuzungumzia ukarabati na uendeshaji wa bwawa la Kalemawe lililopo wilayani Same mkoani Kilimanjaro lililoandaliwa na UNCDF.
DSC_0038
Pichani juu na chini ni Mkuu wa ushauri wa ufundi wa Mfuko wa Umoja wa mataifa wa Ukuzaji Mitaji (UNCDF), Bw.  Peter Malika (kulia) akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Same, Herman Kapufi kufungua rasmi kongamano hilo.


DSC_0096
Washiriki wakitamaza video ya bwawa la Kalemawe lililopo wilayani Same mkoani Kilimanjaro kujionea hali halisi ya bwawa hilo linalohitaji ukarabati.
20140626_124736
muonekano wa bwawa la Kalemawe lililopo wilayani Same mkoani Kilimanjaro wakati UNCDF walipotembelea eneo hilo.
ZAIDI ya watu  10,000 wanaozunguka bwawa la Kalemawe wilayani Same mkoani Kilimanjaro watanufaika na  ukarabati wa bwawa hilo na kuwekewa muundo mpya wa kiutawala  na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Ukuzaji wa Mitaji  (UNCDF).
Bwawa hilo ambalo lipo katika kata za Kalemawe na Ndungu lilijengwa na watawala wa Kiingereza mwaka 1952-1959  kwa ajili ya kusaidia shughuli za kilimo na ufugaji  baada ya kuanzishwa kwa hifadhi ya Mkomazi na hivyo wakazi kuzuiwa kwenda katika hifadhi hiyo kwa shughuli mbalimbali.
Taarifa ya kuwepo kwa mradi huo mkubwa, imetolewa na Mkuu wa ushauri wa ufundi wa Mfuko wa Umoja wa mataifa wa Ukuzaji Mitaji (UNCDF) nchini, Bw. Peter Malika wakati akiwakaribisha madiwani wa kata hizo ambao wameitwa katika kongamano la siku moja Dar es salaam kuzungumzia ukarabati na uendeshaji wa bwawa hilo.
Malika amesema Mfuko huo wa ukuzaji wa mitaji unasaidia ukarabati wa bwawa hilo kupitia mpango wake wa uendelezaji rasilimali kwa kutumia fedha za ndani (LFI) .
Amesema baada ya ukarabati huo,  mradi utaendeshwa kwa pamoja kati ya serikali na watu binafsi.
Malika alisema ukarabati huo unakidhi lengo la mfuko ambalo ni kuwezesha miundombini inayoleta maendeleo.
 “Ukarabati na hatimaye uendeshaji wa bwawa hilo kutasaidia kuleta mabadiliko makubwa ya maendeleo ya mitaji kwa watu binafsi na umma.” alisema
 
 

UN YAZINDUA RIPOTI YA DAWA ZA KULEVYA DUNIANI

Uongozi wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) umezindua ripoti ya Kupambana na dawa za kulevyaa ya Umoja wa Mataaifa, Uzinduzi uliofanywa Machi 4, Jijini Dar es Salaam.
 
Wakizungumza mbele ya wandishi wa habari kwa upande wake, Afisa Habari wa Kituo Cha Habari wa Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vuzo alibainisha ripoti hiyo imeweza kuchambua mambo mbalimbali dhidi ya dawa za kulevya na mikakati iliyofikiwa.
 
Ambapo alisema kuwa miongoni mwa mambo yaliyomo kwenye ripoti hiyo ni pamoja na kupungua kwa wimbi la kuingia kwa dawa za kulevyaa nchini hasa kupitia njia za bahari ya Hindi huku mji wa Mexico wa America, ukipunguza kwa asilimia kubwa matumizi ya dawa za kulevya.
 
Vuzo alibainisha kuwa, pia mikakati iliyofikiwa ambayo pia imo kwenye ripoti hiyo ni pamoja na mfumo wa kuwasaidia watumiaji wa dawa za kulevya wanaoacha kwa kuwapatia dawa maalum za kupunguza taratibu matumizi hayo.
DSCN9301
 Mchambuzi Mkuu wa Mifumo ya Kompyuta wa Tume ya Taifa ya kudhibiti  Ukimwi (DCC), January Ntisi akionyesha ripoti hiyo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani).
 
‘Mipango ya kuwapatia wale wanaocha dawa maalum za kusaidia utumiaji wa madawa na pia dhidi ya kupambana na dawa maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi wa watumiaji” alisema Vuzo.
 
Aidha, alibainisha kuwa,  Afrika Kusini katika bara la Afrika ndio inayoongoza kwa kuwa na njia nyingi za usafirishaji wa dawa za kulevya aina ya Cocaine na Heroine .


DSCN9317
Mchambuzi Mkuu wa Mifumo ya Kompyuta wa Tume ya Taifa ya kudhibiti  Ukimwi (DCC), January Ntisi akifafanua jambo na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo.
DSCN9311
Baadhi ya waandishi wa habari na wadau wa kupambana utumiaji wa Madawa ya Kulevya waliohudhuria uzinduzi huo.

DSCN9299
Mchambuzi Mkuu wa Mifumo ya Komputa wa Tume ya Taifa ya kudhibiti  Ukimwi (DCC), January Ntisi akizindua kitabu cha ripoti ya Bodi ya Kupambana na Dawa za Kulevya ya Umoja wa Mataifa, kwenye hafla ya uzinduzi uliofanyika Machi 4, MAELEZO, jijini Dar es salaam. Kushoto ni Afisa Mipango wa Umoja wa Mataifa, Immaculata Malyamkono-Nyoni na katikati ni Makamu Mwenyekiti wa Mtandao wa Kupambana na Watumiaji wa Madawa ya Kulevya,Very Kunambi.

DSCN9305
Afisa habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na uzinduzi wa ripoti ya Kupambana na dawa za kulevya ya Umoja wa Mataifa. Kulia ni mgeni rasmi Mchambuzi Mkuu wa Mifumo ya Kompyuta wa Tume ya Taifa ya kudhibiti  Ukimwi (DCC), January Ntisi na kushoto ni Afisa Habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Usia Nkhoma Ledama.


 

Wednesday, March 4, 2015

OLOLOSOKWAN WAFURAHIA UJIO WA KIJIJI CHA DIGITALI, UNESCO WATOA MAFUNZO


DSC_0057
Mkurugenzi wa Shirika lisiolo la kiserikali la IrikRAMAT linalomiliki Redio Loliondo FM, Bw. Yannick Ndoinyo akitoa maoni yake wakati wa kuhitimisha warsha ya wiki moja iliyomalizika mwishoni mwa wiki wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani ikiwa ni sehemu ya mandalizi ya utekelezaji wa mradi kijiji cha Kidigitali (Unesco-Samsung Digital Village) cha Ololosokwan kilichopo wilayani Ngorongoro mkoani Arusha. Warsha hiyo ya wiki iliandaliwa na Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO)nchini.


DSC_0070
Picha ya pamoja na washiriki wa warsha hiyo ya wiki moja iliyomaziki mwishoni mwa juma wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.

DSC_0070
Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO, Zulmira Rodrigues akitoa maboresho ya kazi za vikundi vilivyokuwa vikijadili na kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali zilizopo katika kijiji cha Ololosokwan kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kijiji cha kidigitali.

DSC_0118
Mkurugenzi mkazi wa shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akisikiliza baadhi ya maboresho ya changamoto zilizojadiliwa na kikundi kazi cha sekta ya elimu na wadau mbalimbali wa elimu.

DSC_0064
Mkurugenzi mkazi wa shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues, akionesha kwa mifano baadhi ya bidhaa za nje zikivyokuwa na ubora kwenye vifungashio wakati wa warsha ya wiki moja inayoendelea wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya utekelezaji wa mradi wa kijiji cha digitali (Unesco-Samsung digital village) kwa wakazi wa kijiji cha Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.

DSC_0008
Kutoka kushoto ni Mathias Herman wa UNESCO, Mkurugenzi wa elimu ya msingi kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Sarah Mlaki pamoja na Afisa Mtendaji wa kijiji cha Ololosokwan, Emmanuel Madeje.
DSC_0066
Pichani jii na chini ni wadau mbalimbali wa elimu, afya, Tehama na masuala ya utamaduni na uchumi waliohudhuria warsha ya wiki moja iliyoandaliwa na UNESCO wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani.
DSC_0054
Afisa Miradi msaidizi kutoka UNESCO, Myoung Su Ko (kushoto) na Afisa Maendeleo wa Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro Teresia Irafay wakinakili yanayojiri wakati wa kuhitimisha warsha ya wiki moja ikiwa ni sehemu ya mandalizi ya uwapo wa kijiji cha kidigital (Unesco - Samsung digital village) katika kijiji cha Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.

DSC_0051
Ofisa Ustawi wa jamii Ngorongoro, Beneth Bwikizo akitoa neno la shukrani kwa niaba ya ujumbe wa kijijini cha Ololosokwan uliohudhuria warsha hiyo ya wiki moja iliyomalizika mwishoni mwa juma wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.
DSC_0018
Mwenyekiti wa kikundi kazi cha sekta ya afya kutoka UNESCO, Bw. Mathias Herman akiwasilisha mrejesho wa kikundi kazi chake wakati wa kuhitimisha warsha ya wiki moja ya maandalizi ya utekelezaji wa mradi wa kijiji cha kidigitali (Unesco-Samsung Digital Village) cha Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
DSC_0036
Mratibu wa shirika la IrikRAMAT  Foundation, Salangat Mako akitoa mrejesho wa suluhu za changamoto mbalimbali za kikundi cha uchumi na utamaduni wakati wa kuhitimisha warsha hiyo ya wiki moja.
DSC_0044
Mwenyekiti wa kikundi kazi cha sekta ya elimu kutoka UNESCO, Jennifer Kotta akitoa mrejesho wa kilichojadiliwa na kikundi chake.
DSC_0003
Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa kikundi kazi cha sekta ya Tehama,  Al Amin Yusuph akiwasilisha mrejesho wa kazi ya kikundi chake wakati wa kuhitimisha warsha ya wiki moja ikiwa ni sehemu ya mandalizi ya utekelezaji wa mradi wa kijiji cha kidigitali Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoani Arusha
Na Mwandishi Wetu
WAKAZI wa kijiji cha Ololosokwan wamesema kwamba ujio wa kijiji cha digitali katika kijiji chao ni neema kwao kwani kitawasaidia kukabiliana na changamoto kubwa za maisha zinazowakabili.
Kauli hiyo wameitoa mwishoni mwa wiki wakati wa kuhitimisha warsha ya siku saba ya kuangalia fursa na changamoto zitakazoambatana na mradi huo wa miaka mitatu unaodhaminiwa na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO)  kwa kushirikiana na kampuni ya Ki-elektroniki ya Samsung.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi wenzake waliohudhuria warsha hiyo ambapo wataalamu mbalimbali wanaohusika na mradi huo walikutana kujadili changamoto na namna ya kukabiliana nazo, Salangat Mako, alisema kwamba tatizo la miundombinu, Afya na Elimu wanaamini litakabiliwa na mradi huo.
Alisema  kuna shida kubwa ya elimu kutokana na mazingira yaliyopo ambapo wanafunzi wanalazimika kutembea kilomita 14 kwenda na kurudi shule hali inayodhoofisha ari ya kujifunza.
Aidha alisema kwamba kuna changamoto katika zahanati yao yenye wauguzi wawili  huku hospitali ya wilaya ikiwa kiasi cha kilomita 50 hali inayowafanya watu wengi kutegemea mitishamba katika matibabu mbalimbali pamoja na wanawake kusaidiwa uzazi na wakunga wa jadi.
Alisema kuwepo kwa mradi huo kutasaidia wanafunzi kuweza kujisomea kwa kutumia mfumo wa mtandao wa intaneti na hivyo kuwa katika nafasi ya kuelimika vyema kutambua wajibu wao na fursa zilizopo  zinazowazunguka kwa kuwa hifadhini.
Aidha kuwepo kwa kiliniki ya mtandao kutaongeza ufanisi wa zahanati iliyopo pamoja na kuipa mkono katika tiba na kuondoa watu kutegemea tiba za asili.
Akizungumzia fursa za kiuchumi alisema ni matarajio yao kwamba kuwepo kwa kijiji hicho na utamaduni wake, kutawezesha kutumia vyema fursa za kitalii ili kukua kiuchumi kwa kujua mipango inayostahili katika kuendeleza utamaduni kwa jicho la kibiashara zaidi.
Naye Mganga mfawidhi wa zahanati ya Ololosokwan Obeid Laizer ambaye yupo katika kijiji hicho kwa miaka 15 amesema ana matumaini makubwa na mradi huo kwa kuwa mchanyato wake unaonekana kujali zaidi sosholojia za watu na afya zao hasa kwa kuwa na kliniki inayotembea na tiba kwa intaneti itakayomuwezesha kuwasiliana na madaktari wenzake ili kupata ufumbuzi wa matatizo ya afya.
Alisema kwamba kijiji hicho kina magonjwa mengi japokuwa makubwa ni nyumonia, ukosefu wa damu, magonjwa ya zinaa, majereha ya wanyama kutokana na kuchunga mbugani na ugonjwa wa kuhara damu.
Alisema uwapo wa maabara utawasaidia kupata uhakika wa tiba kuliko sasa ambako wanafanya kwa kukisia zaidi.
Naye Ofisa Ustawi wa jamii Ngorongoro Beneth Bwikizo amesema kwamba mradi huo utaleta mabadiliko makubwa kwa wanakijiji hapo kutokana na shughuli nyingi za hapo kuhusanishwa na mradi huo.
Alisema mradi huo ambao unaangalia zaidi kukabili utamaduni unaokwamisha maendeleo kwa kutoa elimu na kuiunganisha na dunia nyingine kwa mawasiliano unaonekana utafanya maisha ya wakazi wa hapo kuboreka.
Alisema mradi huo wa kwanza nchini Tanzania na watatu bara la Afrika umempa hamasa kubwa baada ya kuona unaangalia changamoto zilizopo Ololosokwan ambazo ni za miundombinu katika elimu, afya na uchumi na kuzifanyia kazi.