Monday, April 29, 2013

PADRI ADAIWA KUFUMANIWA NA MKE WA MTU, ANAJULIKANA KWA JINA LA MAMA P.....

Padri Urbanus akihamaki baada ya kuvamiwa ndani ya chumba chake ndani ya parokia na kupigwa picha akiwa anavunja amri ya saba na mke wa mtu

hapa Padri akiomba msamaha asidhuriwe  baada ya kufumaniwa akijifaidia mke wa mtu ndani ya Parokia

Baada ya picha kupigwa hapa wakaruhusiwa kuvaa nguo,  Mama P anaonekana akivaa sidiria aka kificha manyonyo, na Padri akivaa boxer yake

wakiwa hawaelewi cha kufanya


KANISA Katoliki Jimbo la Moshi limeingia katika kashfa nzito baada ya padri wake, Father Urbanus Ngowi wa moja ya parokia zake kudaiwa kufumaniwa na mwanamke anayesemekana ni mke wa mtu, Ijumaa Wikienda lina sakata zima.
Sakata la fumanizi hilo linadaiwa kutokea Jumatatu ya wiki iliyopita chumbani kwa padri huyo, Marangu Wilaya ya Moshi Vijijini ambako Father Ngowi inasemekana alikutwa ‘laivu’ akiwa na mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la kijamii la Mama P.
Pamoja na kunaswa huko, vyanzo havijaeleza humo chumbani wawili hao walikuwa wakifanya nini!
Habari zinadai siku ya tukio, mwanamke huyo aliingia nyumbani kwa padri huyo ambapo baadhi ya ndugu wa mumewe walikuwa wakimfuatilia baada ya madai yaliyokuwepo kwamba ana ukaribu wenye maswali mengi na mtumishi huyo wa Mungu.
“Unajua siku nyingi ilivuma kwamba Mama P na Father Ngowi wana ukaribu wenye maswali mengi, mume wake alifuatilia na kubaini ni kweli lakini akashindwa kuutenganisha ukaribu wao,” kilidai chanzo.
Chanzo kikaendelea kudai kwamba baada ya kuona mkewe amejikita kwa mtumishi wa Mungu, mumewe (jina tunalo) alinyoosha mikono juu na kumwachia Mungu.
Chanzo: Sasa siku hiyo baada ya ndugu wa mume kumfuatilia mpaka anaingia kwa Father Ngowi, wakaona ni bora watafute mpigapicha ili kupata picha za tukio ambazo zitakuwa ushahidi siku za mbele.
“Walipompata wakazama ndani, sekeseke likaanzia hapo. Walimkuta mwanamke huyo na mtumishi wa Mungu wapo kitandani.”
AWEKWA KITIMOTO
Habari zinadai kwamba kufuatia tukio hilo, tayari Kanisa Katoliki limemweka kitimoto padri huyo ambaye alikuwa akihudumu katika Parokia ya Korongoni, Moshi Vijijini kabla ya kuhamishwa na kupelekwa Parokia ya Makomu, Marangu ambako inadaiwa ameshushwa cheo.
Inadaiwa kuwa baada ya tukio hilo, Father Ngowi alikana kukutwa na mke wa mtu chumbani kwake lakini alipobanwa sana na mabosi wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki Moshi, alikiri na kudai ibilisi alimpitia na kuomba kanisa limsamehe na kutompa adhabu kali ambayo itamuathiri kisaikolojia.
Hili ni tukio kubwa na la aina yake kuwahi kulikumba Kanisa Katoliki nchini kwa padri wake kudaiwa kukutwa na mke wa mtu chumbani kwake!
SIKU ZA NYUMA
Kuna madai kwamba mwaka jana (2012), Father Ngowi, mbele ya waumini wake alisoma barua yenye kukana shutuma zote zilizoelekezwa kwake kwamba amekuwa na ukaribu wenye maswali mengi na wake za watu.
Taarifa zilidai kuwa padri huyo aliweka wazi akisema si kweli kwamba amekuwa na ukaribu unaotajwa, akawataka waumini wake wapuuze tuhuma hizo alizosema zina mwelekeo wa kuchafua sifa yake na taswira ya Kanisa Katoliki kwa jumla.
Hayo ni madai ya vyanzo vyetu ambavyo viliambatanisha na picha mbalimbali za tukio hilo lenye kushtua waumini sambamba na namba za simu za padri huyo kwa ajili ya mawasiliano ili kujiridhisha.
IJUMAA WIKIENDA NA FATHER NGOWI SASA
Baada ya kujazwa madai hayo, kama ilivyo desturi ya Magazeti ya Global Publishers likiwemo hili (Ijumaa Wikienda), lilimsaka Father Ngowi kwa udi na uvumba ambapo Ijumaa iliyopita nyakati za mchana lilifanikiwa kuzungumza naye lakini kabla ya kufanya hivyo, kifaa cha kunasia sauti kiliwekwa sawa na mambo yalikuwa hivi:
Wikienda: Haloo, naongea na Father Ngowi wa Parokia ya Korongoni, Marangu, Moshi?
Father Ngowi: Naam ni mimi, nani mwenzangu?
Wikienda: Naitwa…(mhariri anataja jina), napiga simu kutoka Magazeti ya Global Publishers.
Father Ngowi: Uko wapi?
Wikienda: Makao Makuu ya Global Publishers, Dar es Salaam.
Father Ngowi: Eeh…unasemaje?
Wikienda: Kuna madai ya wewe kukutwa na mke wa mtu chumbani. Je, unaweza kunielezea kama ni kweli na tukio lilikuwaje?
Father Ngowi: Siyo mimi.
Wikienda: Wewe siyo Father Urbanus Ngowi?
Father Ngowi: Nimekwambia siyo mimi, hao ni matapeli wanataka pesa ndiyo wametengeneza hizo picha.
Wikienda: Kwa hiyo unataka kuniambia hizi picha ni za kutengeneza?
Father Ngowi: Nimekwambia hao ni matapeli wanataka pesa.
Wikienda: Ulishaziona picha zenyewe?
Father Ngowi: Sijui.
NGOMA YATUPWA KWA MKUU WA JIMBO
Wikienda: Mbona tayari tukio hilo linadaiwa limeshafika kwenye ngazi ya jimbo, Moshi kwa Father Paul Uria?
Father Ngowi: Muulize yeye ndiye mkubwa wangu.
Wikienda: Basi nisaidie namba yake ya simu ya mkononi.
Baada ya takribani dakika 10, Father Ngowi alituma namba ya simu ya Father Uria na mambo yakawa hivi:
Wikienda (huku kinasa sauti kikiendelea kufanya kazi): Haloo…naitwa …(mhariri anajitambulisha) kutoka Magazeti ya Global Publishers, Dar es Salaam, naongea na Mkuu wa Jimbo Kanisa Katoliki, Moshi, Father Uria?
Father Uria (kwa sauti yenye unyenyekevu): Ndiyo.
Wikienda: Una taarifa za mtumishi wako, Father Ngowi kunaswa na mke wa mtu chumbani?
Father Uria: Kwanza mimi si mkuu wa jimbo, ni mwakilishi wa mkuu wa jimbo. Sipo mjini kwa sasa nipo Kilema huku vijijini kwenye huduma lakini nilikuta ‘missed calls’ zake jana (Alhamisi) kwani ilikuwa tukutane kwa sababu alishanijulisha kuwa kuna tukio kama hilo unaloniambia wewe.
NGOMA YAWA NZITO, YATUPWA LEO JUMATATU
“Kweli tulikuwa tukae jana lakini ikashindikana, leo (Ijumaa) ni sikukuu (Muungano), kesho (Jumamosi) na keshokutwa (Jumapili) ni wikiendi. Kwa hiyo tutakaa Jumatatu (leo) hivyo nipigie saa 10:00 jioni siku hiyo ili nikupe maagizo tutakayofikia na mengine.
Wikienda: Lakini Father Ngowi alikueleza tukio lilikuwaje?
Father Uria: Nimekwambia tukikaa ndiyo tutajua kilichotokea. Wewe nipigie hiyo saa 10 nikupe kitakachojiri.
Wikienda: Shukrani Father Uria kwa ushirikiano.
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS

MBUNGE LEMA AACHIWA KWA DHAMANA YA MILIONI MOJA, APANDISHWA KIZIMBANI KWA MADAI YA KUMKASHIFU RC MULONGO KWA MANENO KWAMBA 'ANATEMBEA KAMA ANAENDA KWENYE SENDOFF'

wafuasi wa CHADEMA wakimsikilia Lema

Wafuasi wa CHADEMA wakimsikiliza Mbunge wao Godbless Lema alipokuwa akiwahutubia leo katika viwanja vya shule ya msingi ngarenaro

wafuasi wa chadema wakiwa wamezingira viwanja vya mahakama kuu jijini hapa
Mama mmoja shabiki wa CHADEMA akionyesha bango lenye maandishi kuonyesha hisia zake kwa Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema.

Umati wa mashabiki wa CHADEMA jimbo la Arusha wakimsikiliza mbunge wao Godbless Lema baada ya kutoka mahakamani, hapa akiwahutubia wananchi hao katika viwanja vya shule ya msingi Ngarenaro pembeni ya ofisi ya Chadema Mkoa wa Arusha

Mbunge Lema pamoja na Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki Joshua nasari wakiwa juu ya gari wakihutubia umati wa wananchi waliojitokeza baada ya kupata dhamana kwa kosa la kukashifu
Kwa mujibi wa waendesha mashtaka wa Serikali, Mambo yaliyomfanya Mbunge wa arusha Godbless Lema akamatwe na kunyimwa dhamana  ni haya yafuatayo;

i)Kosa la kwanza ni kuwaambia wanafunzi wa chuo cha uhasibu alipoenda kuwatuliza kuwa ‘dhambi kubwa kuliko zote ni woga ‘. Haki hutafutwa na kupiganiwa ikiwa jambo unalipigania ni la msingi na linafaa kupiganiwa (Worth fighting for)

ii)Kosa la pili ni pale alipotamka kuwa ‘’Tumemtafuta mkuu wa mkoa juu ya Matatizo yenu na mlivyoshuhudia hapa amechukua muda mrefu na kuingia kama vile anaingia kwenye send-off.Hawa ndiyo viongozi wetu ambao hawajali matatizo ya wananchi’’
iii)Kosa la Tatu ni pale alipotamka kuwaambia wanafunzi kuwa ‘’Mimi Mbunge wenu nipo sambamba nanyi hadi mpate haki yenu na ikiwa mkuu wa mkoa hatakuja hapa kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wa mkoa nitawaongoza hadi ofisini kwake ili mpate majibu na haki yenu kwani ni haki yenu ya msingi kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo niliapa kuilinda Bungeni na pia inaruhusiwa kwa mujibu wa kikanuni na kifalsafa katika utekelezaji wa utawala bora wa kidemokrasia ambao msingi wake ni kusikilizwa na kulinda haki za binadamu’’

Saturday, April 27, 2013

KIZIMBA CHA MAGAZETI LEO JUMAMOSI 27.04.2013













MWANDISHI MBWAMBO ASITULETEE TENA `UMBILIKIMO` WAKE WA FIKRA KATIKA UKURASA HUU.



Na Mwandishi Wetu

Mwenyekiti General Ulimwengu,aliwahi kusema `Raia Mwema ama Raia Muungwana ni Yule anayeamka asubuhi na kujiona ni mwenye afya njema ,kisha anampigia simu daktari wake na kumuuliza hatma ya afya yake kwa miaka mitano ama kumi ijayo.(Ntafafanua).

Nimekuwa mmoja wa `waumini` wazuri wa gazeti la Raia Mwema kwa muda mrefu sasa,nemepata mengi na kujifunza mengi kupitia makala mbalimbali zinazopewa nafasi katika gazeti hili hasa kwa Makala zinazoandikwa na Waandishi waliyobobea kama Johnson Mbwambo ambaye ameanza `kuzeeka vibaya`.

Toka nipo Shule ya Msingi na Mpaka sasa nimekuwa Mwanahabari Bado namsoma Mzee Mbwambo ambaye kwangu nilimuona kama Mwalimu Wangu wa siku nyingi sana bila yeye kujijua,lakini hivi karibuni amenifundisha somo ambalo si tu sijalipenda bali pia sijapata jibu kama Mwalimu Wangu alikuwa `amelewa` wakati anaandika ama  alikuwa ametanguliza hasira za kunyimwa Ukuu wa Wilaya mbele!!!

Katika Raia Mwema Toleo na.292 la April 30,ukurasa wa 11 Kuna  Tafakuri Jadidi Iliyoandikwa na Johnson Mbwambo.Ina kichwa Kikubwa cha Habari kinasema KIKWETE KAWASIFU,SASA WANASHINDANA KUITUKANA CHADEMA! Nimesoma kilichoandikwa na Mwalimu Wangu nikapata shaka na anapoelekea `kiumri`.

Kwakawaida Binadamu kadiri unapoongezeka Umri na ndivyo Busara zinavyoongezeka na ndiyo maana kukawa na msemo usemao `Utu uzima ni dawa`.Mimi ni mmoja wa wanaoamini Mbwambo anaongezeka Umri na siyo urefu,kidogo Napata shaka kuamini kama  ongezeko lake la umri linakwenda sambamba na ongezeko la busara.

Mbwambo amekuwa mshabiki kiasi cha kupitiliza,na kwa kiwango hicho ameshindwa kuthibiti hasira zake na kujitofautisha na hao wabunge wanaotoa lugha `chafu` nayeye ametumbukia humo huku `akijifanya kutumia mgongo wa falsafa za Mwalimu Nyerere.

Katika Makala iliyotoka katika gazeti hili Mbwambo kama kawaida yake ametumia muda mwingi kuwashambulia Wabunge vijana wa chama cha Mapinduzi  kwa madai `eti` wamekuwa wakikikejeli chama chake cha Chadema Bungeni badala ya kuongea mambo ya Msingi.Akasema `eti`wamekuwa wakiwafanya hata Wabunge wa `chama chake ` cha Chadema kujibu kwa Ukali( hakuita ni matusi) eti kwasababu ya Wabunge vijana wa ccm wanaotukana.( ya CCM akaita matusi)

Akiendelea kuandika makala yake Mbwambo kila  mara amekuwa akijikingiliza katika kimvuli cha Mwalimu Nyerere `kinafiki`kujaribu kuhalalisha  maandishi yake yakukitetea chama chake kinachodaiwa kuwa na `udini na ukanda`( Mwambo anatokea Kilimanjaro)

Mbwambo katika maandishi yake akasema (namnukuu) ``Isitoshe,Chadema kiumri si chama kikongwe kama ccm na hivyo katika hali ya kawaida wabunge wa ccm ndiyo wanaopaswa kuonyesha mfano wa uungwana Bungeni kwa wabunge wa Chadema kwakuwa wao wanatoka katika chama kikongwe na kinachokamata serikali kwa miaka mingi`` ( mwisho wa kunukuu)  ``Mzee Mbwambo anamaudhi sana`.

Kwa maandishi yake anataka kutufundisha kuwa wabunge wa Chadema wakitukana tuwaunge mkono kwakuwa wapo katika chama kichanga wala wasikosolewe, na Kwakuwa Chama chao hakishiki Dola basi waachwe tu waporomoshe matusi kama wanavyofanya sasa!!

Yaani Mbwambo anataka Wabunge wa ccm wawe wavumilivu kuvumilia `upuuzi ` wa wabunge wa Chadema . Sitaki kuamini kama Kule kwao Kilimanjaro mtoto akitukana anaachwa kwakuwa bado mdogo ( labda anafanya hivyo kwake) Ndiyo maana Napata shaka na umri wa Mzee Mbwambo unapoelekea! Katika makala yake Mbwambo ameongea mengi yanayokera `kama yeye alivyokerwa na Yule mwandishi aliyemwita `mhandisi anayempigia debe Babu wa Loliondo eti Dawa zake ni tiba sahihi`.

Katika kuifanya Jamii izidi kuiamini taaluma ya Uandishi wa habari ni lazima sisi waandishi wa habari  bila kujali mkongwe ama mchanga tusiwe makatibu waenezi wa vyama vya siasa.

Katika Maandishi  yake Mbwambo anaandika kama vile siyo mwandishi wa habari bali ni `Mwajiriwa wa Chadema`.

Siku zote nimekuwa nikimsoma Mbwambo na kumwelewa na kujifunza kwa kile anachokiandika lakini kwa hili nimeshindwa kuingiza ndani ya ubongo wangu `ushawishi wake` usiyofaa mbele ya jamii kuwa eti watukane wa Chadema,lakini ccm hapana.

Binafsi siungi  mkono lugha chafu zinazotolewa na baadhi ya wabunge bila kujali vyama vyao,sipendi kuona wabunge wanakuwa kichaka cha matusi kwa sisi vijana ama watoto wadogo zaidi yangu kwa namna yeyote ile.

Mbwambo amejielekeza zaidi kuiaminisha jamii kuwa yanayotolewa na Chadema siyo matusi bali ni hoja za msingi na yanayotolewa na baadhi ya wabunge wa ccm siyo majibu ama hoja bali ni matusi.
Mzee Mbwambo amefika mbali zaidi kwa kudai kuwa baadhi ya wabunge wa CCM  wamesifiwa na Rais Jakaya Kikwete na ndiyo maana wamezidi kutukana matusi

Akasema Mwigulu Nchemba alipewa zawadi ya cheo baada ya kukitukana Chadema  na ndiyo maana basi wengine wanaiga ili wapewe zawadi ya vyeo.

Anavyoamini yeye (Mbwambo) CCM wakichaguana katika chaguzi zao kama Chadema basi ni kupeana zawadi za vyeo na siyo haki, CCM wakiteuana kulingana na katiba yao kwa mtazamo wa Mzee Mbwambo huo siyo uteuzi ila ni zawadi baada ya kutukana!

Mzee Mbwambo ameondoka katika uandishi na kuwa mtu wa Propaganda wa Chadema,sitaki kuamini kama kuna mwandishi anayefuata misingi ya taaluma anaweza kuwa na upendeleo kiasi hicho.

Inawezekana kabisa alichokiandika Mzee Mbwambo ni Mawazo yake. Lakini mawazo gani hayo yanayowaza upande mmoja pake yake,mawazo gani ambayo hubadilisha `matusi` kuwa maneno matamu?
Mawazo gani hayo nayaona matusi ya wabunge wa chadema  kuwa ni maendeleo? Huu ni umbilikimo wa fikra ambao hauendi sambamba na heshima alonayo Mzee Mbwambo.

Mzee Mwambo aliwahi kumshambulia Mwandishi mmoja mkoani Arusha akimwita `Mhandisi wa habari` kwa kuwa mwandishi huyo aliandika habari zinazomhusu Babu wa Loliondo na Mwandishi huyo hakuonyesha kuiaminisha jamii kuwa dawa za Babu hazifai.

Alimshambulia mwandishi na kumwelekeza kuwa ni afadhali angeandika habari hiyo kwa mtindo wa kukejeli  ili asionekane kushabikia ushirikina wa Babu.

Sasa Mzee Mbwambo alichokiandika yeye ni afadhali ya huyo Mwandishi aliyemwita `Mhandisi`.
Ameshabikia upuuzi wa baadhi ya wabunge hasa wa chadema,na siwezi kumwita yeye ni `mhandisi`.

Waandishi jamii ya Mzee Mbwambo huko tuendako ni hatari kwa kizazi cha taaluma ya habari.Atawaambukiza ushabiki waandishi wachanga na wanaomsoma ambao watakuwa ni wavivu wa kutafakari kama anavyomaliziaga makala zake kwakusema tafakari.

Binafsi nimetafakari nimebaini umendika kiushabiki,na kama siyo kiushabikia basi pengine unaweza kuwa na una hasira na Rais Kikwete,labda hukupata ukuu wa wilaya nk.tafakari mwenyewe.

Raia Mwema ni Yule anayeamka asubuhi na kujiona ni mwenye afya njema lakini anampigia simu daktari wake akimuuliza hatma ya afya yake miaka kumi ijayo.

Mzee Mbwambo ameamka asubuhi amejiona ni mwenye afya njema,hampigii daktari wake simu anadunda tu barabarani hajui madhara ya baadaye.

Angempigia daktari wake simu angeambiwa maradhi yako ya fikra yanaambukiza hivyo usisambaze maradhi yako ya fikra za upande mmoja kwa watu wote hasa kwa sisi vijana tunaokuwa katika maadili mazuri.

Tafakari…O752 25 01 57…// 0655 2501

Friday, April 26, 2013

UJUMBE WA MBUNGE NASARI KUHUSU KUKAMATWA KWA MBUNGE LEMA

Ujumbe wa Mh Nassari.....


Nimepata kwa mshtuko na nikakataa kuamini kama ni kweli kuwa polisi wa Arusha wamevamia na kuizingira nyumba ya mbunge mwenzangu wa Arusha, Lema.
Nimelazimika kumpigia simu RPC kuthibitisha na cha ajabu akaniambia ni kweli.
Nimemshauri kama kiongozi mwenzake mwenye dhamana ya kusaidia kuilinda kweli na haki ili kuleta Amani ya kweli kwenye mkoa wangu wa Arusha. Sidhani kama ni busara kutaka kuvamia nyumbani kwa Raia mwema achilia mbali Kiongozi mkubwa kama mbunge.
 "Kama watawala wanafanya hivi kwa mti mbichi, itakuwaje kwa mti mkavu" itakuwaje kwa mwananchi wa kawaida anayeishi usa river au unga ltd? Ukifuatilia na kuangalia video ya tukio la uhasibu chuoni arusha, utagundua makosa ya mtawala mkuu wa mkoa, ambaye kimsingi ni mkiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa kuwa sehemu ya sababu ya uvunjifu wa amani, kutokujua hata kusoma saikolojia ya watu.


Nyumbani kwa mbunge hakai mbunge mwenyewe. Kuna watoto akiwemo mwenye umri wa miezi mitano, mke, ndugu etc. Utapigaje mabomu kwenye nyumba hii, bila shaka yatakuwa mauaji. Lema si jambazi, ni kiongozi, ni role model, ni raia mwema sana na mzalendo kwa taifa lake.

Hii wapi sababu ya kuvamia kwake usiku na kuwapa wanafamilia pychological tortue.

Kama amenielewa atasikia, otherwise "truth will always stand" . Tuko tayari na tulishakuwa tayari, hatujashtukizwa. Tunaendelea kuongezewa kura za madiwani arusha juni 16, 2013.
Mbunge Nassari kulia akiwa na mbunge Lema
 Ni vyema watawala wakakumbuka habari ya Farao na Mungu juu ya mateso ya wana wa Israel utumwani. "Mungu akaufanya moyo wa farao kuwa mgumu, ili azidi kujidhihirisha kwa wana wa Israel"

Nassar

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA OFISI YA KAMANDA WA POLISI ARUSHA KUHUSU KUKAMATWA KWA MBUNGE LEMA

mbunge lema akihutubia umati wa wakazi wa Arusha katika moja ya Mikutano yake

TASWIRA SOKO LA MBAUDA LEO ASUBUHI...

Wafanyabiashara wakiuza bidhaa zao pembeni ya barabara

wafanyabishara wakiuza bidhaa zao pembeni ya barabara ya mbauda kwa mrombo leo

Mfanyabiashara wa Kuku akimchinja kuku tayari kwa kuuza

mzee huyu alinaswa na kamera yetu akiwa amebeba kuni, pembeni na soko la Mbauda


Wafanyabiashara wa viatu

Gari hili aina ya Scania lilitumbukia katika mtaro karibu na benki ya Azania na kusababisha foleni kubwa kwa wakazi wanaotumia barabara ya Mbauda kwa Morombo

BREAKING NEWS: MBUNGE LEMA AKAMATWA USIKU WA MANANE, ALALA SERO

Taarifa zilizotufikia hivi punde, Mbunge wa jimbo  la Arusha mjini, Godbles Lema(CHADEMA), amekamatwa na makachero wa jeshi la Polisi usiku wa kuamkia leo na kulazwa sero. Mbunge huyo anatuhumiwa kuhamasisha vurugu katika chuo cha uhasibu IAA zilizopelekea Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo kupopolewa mawe na wanachuo alipokwenda kuwasihi waache vurugu wakati uchunguzi wa kifo cha mwanafunzi mwenzao ukiendelea kufanywa na wapelelezi wa jeshi la Polisi
HABARI ZAIDI ENDELEA KUFUATILIA HAPA!!!!!!!!
Makachero wa jeshi la Polisi wakiwa wamewakamata wanachuo wawili katika vurugu hizo

Baadhi ya wanafunzi waliohisiwa kufanya vurugu chuoni IAA wakiwa chini ya ulinzi ndani ya gari la Polisi

Gari la Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema likivutwa kupelekwa polisi baada ya yeye kutuhumiwa kuchochea vurugu katika chuo cha uhasibu jijini hapa na baadae kutoroka kabla ya kukamatwa leo

Askari wa FFU wakiwa tayari kukabiliana na vurugu za wanafunzi wa chuo cha uhasibu njiro

Askari wa FFU wakiwa wamemweka chini ya ulinzi mmoja wa wanafunzi wa chuo cha uhasibu njiro ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja akituhumiwa kushiriki kwenye vurugu hizo

SAFARI YA MWISHO MWANAFUNZI WA IAA ALIYEUAWA KWA KUCHOMWA NA KITU CHENYE NCHA KALI NA KUFARIKI DUNIA, CHADEMA WATOA TAMKO...

TAARIFA KWA UMMA
MAUAJI YA MWANACHUO WA CHUO CHA UHASIBU ARUSHA (HENRY KAGO) NA KAULI YA CHAFU YA MKUU WA MKOA WA ARUSHA
Ndugu wanahabari na wakazi wote wa mkoa wa Arusha.
Kwanza kabisa, tunapenda kutoa pole za dhati kwa familia, ndugu jamaa, wanachuo na jumuia yote ya chuo cha uhasibu Arusha wa marehemu Henry Kago aliyefariki juzi usiku kwenye tukio la kutisha na kuhuzunisha sana.

Tumesikitishwa na msiba huu na tunawaombea wote Mungu awapatie faraja na utulivu katika kipindi hiki kigumu.

Katika tukio hili, mbunge wa Arusha Mjini Mhe Godbless Lema alijulishwa na kama kiongozi alifika ili kuona namna atakavyoweza kutoa msaada hasa baada ya wanachuo kuonyesha hisia zao kwa vile hawakuona kupata msaada kutoka kwa uongozi wa chuo na serikali kwa ujumla. Hili ni tukio la pili la mauaji ya mwanachuo sambamba na matukio mengi ya wanachuo kuvamiwa na kunyang’anywa mali zao.

Mhe Lema aliwatuliza wanachuo na kuchukua hatua za kumjulisha mkuu wa Mkoa Mhe Mulongo aje na kuzungumza na vijana hawa.

Hata hivyo ujio wa mhe Mulongo ulionekana haukuwa na dhamira ya dhati na badala yake alionyesha madharau makubwa ambayo mpaka sasa nashindwa kuelewa alikuwa na maana gani kuonyesha tabia ya kipuuzi namna ile kwa vijana waliokuwa wamepata msiba wa mwenzao.

Picha za video zinaonyesha kwa dhahiri jitihada kubwa aliyoifanya mhe Lema kuwatuliza vijana hawa na kuwaomba wawe wavumilivu.

Baada ya tukio zima kukumbwa na vurugu ambazo kimsingi chanzo ni tabia aliyoinyesha Mhe mulongo kwa vijana hawa, mkuu wa mkoa aliongea na waandishi wa habari kuwa chanzo cha vurugu hizo ni Mhe Lema na kuwa tukio zima la mauaji haya ni masuala ya kisiasa na kuwa wanasiasa wamepanga mambo haya ili kujipatia umaarufu, hii na kauli ya mwendawazimu kabisa. 

Katika hatua hii walimkamata Wakili Mhe Albert Msando ambaye pia ni diwani wa CHADEMA na kumchukua kwa mahojiano.

Kwa ujumla msingi wa suala la kumtafuta muuaji wa Henry umepabadilika na kuwa kumtafuta Lema.

Tunataka tuweke kumbukumbu hii kwa wakazi wa Arusha, jambo hili ni mfululizo wa matukio mengi yasiyoonyesha weledi ya Mhe mulongo ambayo amekuwa akifanya na kama chama tunamtakia hivi kikombe kitakopajaa atatambua maana ya nguvu ya umma.

 Anaweza kudharau maneno haya, afanye hivyo kwa vile anajisikia kuwa yupo na mamlaka ya kiserikali lakini tunarudia kusema kuwa kamwe hatuwezi kuendelea kuvumilia uongo na akili mbovu za namna hii kuongoza watu wenye akili. Narudia kusema hatutavumilia uongo wa namna hii kuendelea kusemwa halafu familia iliyopoteza mtoto wao mpendwa ikiwa katika masononeko makubwa.

Sasa mhe Mulongo na watu wake wajiandae vema maana tumejiandaa kupambana na watu na/au viongozi ambao tumeshajua ni wapotoshaji na wahuni na wanafanya mambo ya kihuni.

Tunawaomba wakazi wa Arusha wawakatae viongozi wapotoshaji na wahuni, wasiwape ushirikiano wowote ule na sisi tutasimama na wananchi kwa pamoja katika mazingira yote ili kudumisha uongozi bora wenye kujali na kuheshimu raia wote kwa mustakabali wa mkoa wetu kiuchumi na katika kujenga utulivu.
Imetolewa leo tarehe 25 Aprili 2013
Amani Golugwa
KATIBU WA CHADEMA – KANDA YA KASKAZINI.
NI majonzi: wanafunzi wa chuo cha IAA wakitoa salamu zao za mwisho

Wanafunzi wakitoa salamu zao za mwisho

Mmoja wa watumishi wa chuo cha IAA akitoa salamu zake za mwisho kwa marehemu

Wanafunzi pamoja na watumishi wa chuo cha IAA wakitoa salamu zao za mwisho

Wanafunzi wa Chuo cha uhasibu njiro IAA, wakitoa mwili wa marehemu nje ya chumba cha kuhifadhia maiti kabla ya kutoa salamu za mwisho na kusafirishwa nyumbani kwao Iringa kwa mazishi

Thursday, April 25, 2013

MKEMIA MKUU WA SERIKALI ATOA SOMO KUHUSU DNA KWA MAAFISA UPELELEZI WA MIKOA YA ARUSHA, MANYARA, KILIMANJARO NA SINGIDA

Afisa upelelezi katika ofisi ya RCO jiji la Arusha, Tausi Abdallah akiwa amepokea cheti chake, nyuma ni afisa mwingine wa Polisi
Mkemia Mkuu wa Serikali Samwel Manyele akimkabidhi cheti cha ushiriki wa mafunzo ya DNA Afisa Upelelezi wa jeshi la Polisi Arusha, Tausi Abdallah jana jijini hapa
Na Mwandishi Wetu, ARUSHA

UKOSEFU wa maabara ya wakala wa Mkemia mkuu wa Serikali mikoani
kumekuwa kukisababisha usumbufu kwa wadau wa huduma hiyo kusafirisha
sampuni hadi Jijini Dar es salaam, kungojea majibu kwa muda mrefu na
gharama kubwa ya kusafirisha sampuli hizo.

Hayo yalielezwa jana jijini hapa na Afisa Tawala wa Mkoa wa Arusha
Eveline Mtamisa alipokuwa akifungua warsha ya siku mbili kwa wadau wa
huduma hiyo kutoka Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Singida.

Alisema kutokamilika kwa maabara ya mkemia mkuu jijini Arusha
itakayokuwa ikihuduma wadau wa kanda ya kaskazini kunapunguza ufanisi
na kupunguza matumaini ya wadau wa huduma hiyo kupata huduma kwa
wakati za zenye ubora wanaoutarajia.

“Naomba tatizo hili liundiwe mkakati ili maabara hii ianze kutumika na
kuondoa matatizo ya kusafirisha sampuni kwenda Dar es salaam,
kumbukeni mkoa wa Arusha una umuhimu wa pekee kitaifa na kimataifa,
ofisi nyingi za Kimataifa ziko hapa,”alisema.

Alisema Jumuiya za Kimataifa zilizopo jijini Arusha zinahitaji huduma
ya wakala wa Mkemia wa Serikali kwa ukaribu na kwa ufanisi ili Jumuiya
hizo ziridhike kuwepo kwa ufanisi wa hali ya juu wa huduma hiyo
nchini.

Mtamsa aliwataka wadau wa huduma hiyo kutoka vyombo vya usalama kuwa
waadilifu katika kutekeleza majukumu yao na kuondoa kero ya wao
kupokea rushwa ambayo imekuwa ikielekezwa kwao kila mara.

Kwa upande wake Mkemia Mkuu wa Serikali Samweli Manyele alisema ofisi
yake imejipanga kuhamasisha wadau mbalimbali nchuini kutumia huduma
hiyo ili kuboresha utekelezaji wa huduma zao bila shaka.

Washiriki wa mafunzo kuhusu vinasaba wakimsikiliza kwa makini Mkemia Mkuu wa Serikali Samweli Manyele alipokuwa akifunga mafunzo hayo ya siku mbili yaliyoanza Aprili 23 hadi 24, Mwaka huu

Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali jijini Arusha wakimhoji Mkemia Mkuu wa Serikali, kuhusu mkutano uliokuwa ukiendelea katika hoteli ya Naura spring jijini Arusha

Washiriki wakisikiliza kwa makini

Washiriki wakisiliza kwa makini hotuba ya mkemia mkuu Samweli Manyele

Washiriki wa mafunzo kuhusu shughuli mbalimbali ikiwemo namna ya uchukuaji wa sampuni za vinasaba DNA kutoka idara ya upelelezi ya jeshi la polisi jijini Arusha, katika picha ya pamoja.  wa pili kutoka kulia ni Rashida Nchimbi ( Mwandishi wa jeshi la Polisi jijini Arusha), na wanne kutoka kulia ni Tausi Abdallah anayefanya kazi ofisi ya RCO Mkoa wa Arusha 






KIFO CHA MWANAFUNZI CHUO CHA UHASIBU NJIRO CHASABABISHA VURUGU, MBUNGE LEMA ASAKWA KWA MADAI YA KUCHOCHEA VURUGU

MWANAFUNZI wa mwaka wa pili  katika chuo cha uhasibu  kilichopo Njiro jijini Arusha,Henry Koga anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka (25 hadi 30) ameuawa kinyama kwa kuchinjwa na kisu shingoni na kundi la watu wasiofahamika wakati wakitoka kwenye kumbi za starehe na wenzake.

Kufuatia tukio hilo ,kundi la wanafunzi walileta vurugu kubwa na kukataa kutii amri ya mkuu wa mkoa wa Arusha,Magesa Mulongo ya kuwataka warudi darasani wakati hatua zaidi za kisheria zikichukuliwa huku wakimzomea,hali iliyosababisha polisi kuingiliaka kali na kuwafyatulia mabomu zaidi ya 50 na baadhi yao kujeruhiwa.

Tukio la kuuawa kwa mwanafunzi huyo limetokea  majira ya saa 4 usiku wa kuamkia leo ambapo marehemu huyo akiwa na wenzake walivamiwa na kundi la wahuni wapatao wanne katika eneo la CDA ,umbali mchache kutoka eneo la chuo hicho na kumchoma kisu shingoni .

Hata hivyo jitihada za wenzake kutaka kuokoa maisha yake kwa kumkimbiza hospitalini, zilishindikana kwani alifariki dunia muda mfupi baada ya tukio hilo kutokana na kuvuja damu nyingi.

Aidha wanafunzi hao walijikusanya asubuhi yake na kuanza kuandamana  kushinikiza uongozi wa chuo hicho kutoa tamko juu ya vitendo vya uhalifu vinavyojirudia mara kwa mara katika chuo hicho  bila kuchukuliwa hatua zozote na kufanya maisha ya wanachuo hao kuwa hatarini.

Wanafunzi hao walisikika wakilalamikia hali  ya ukimya wa viongozi kushindwa kudhibiti matukio ya uhalifu kwani mwishoni mwa mwaka jana mwanafunzi mwingine aliuawa na vibaka kwa kuchomwa na kisu pia wanafunzi hao waliwahi kuvamiwa  chuoni wakiwa wamelala na kuporwa vitu mbalimbali ikiwemo laptop simu na fedha.

Wakati vurugu za wanafunzi zikiendelea alifika mkuu wa mkoa wa Arusha ,Magesa Mulongo na kuwasihi waache vurugu na wakubali kumsikiliza hata hivyo wanafunzi hao zaidi ya 500 walianza kumzomea huku baadhi yao wakionekana kurushia mawe

Mkuu wa mkoa alilazimika kuondoka eneo hilo ,hatua iliyowalazimu askari wa kutuliza ghasia kufyatua mabomu ya machozi kwa lengo la kuwatawanya na kujikuta baadhi yao wakijeruhiwa vibaya .

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Arusha ,Ibrahimu Kilongo alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa  wanafunzi zaidi ya 7 wanashikiliwa katika vurugu hizo huku uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea .

Mkuu wa mkoa Magessa Mulongo pamoja na timu yake wakiingia katika eneo la shule ambapo aliambulia zomea zomea ,kurushiwa mawe,lugha za kejeli kutoka kwa wanafunzi hao kwa kile wanachodai kuwa serikali imekuwa siyo sikivu kutatua matatizo yao ya mara kwa mara ikiwepo kuibiwa vitu mbalimbali




ASKARI WA FFU WAKIWA TAYARI KUDHIBITI VURUGU CHUONI HAPO

UMATI WA WANAFUNZI WA CHUO CHA UHASIBU NJIRO IAA WAKIMSIKILIZA MKUU WA MKOA MAGESA MULONGO KABLA YA KUANZISHA VURUGU WAKIPINGA MWANAFUNZI MWENZAO KUUAWA