Friday, June 28, 2013

BARAZA LA HABARI LAKUTANA NA WANAFUNZI AJTC, LATOA ONYO KWA WAHARIRI, WAANDISHI, WATAKIWA KUFUATA WELEDI KATIKA KUANDIKA HABARI ZAO



Na Mwandishi wetu, Tanzaniasasa

WAKUFUNZI wa vyuo vinavyotoa elimu ya uandishi wa habari nchini wametakiwa kuwafundisha kwa ufasaha wanafunzi wao maudhui yaliyopo katika azimio Dar es salaam kuhusu uwajibikaji na uhuru wa vyombo vya habari (DEFIR), ili kutengeneza waandishi watakaofuata maadili ya habari na kuwa kioo kwa jamii.

Wito huo umetolea leo jijini hapa na Meneja utafiti na machapisho wa Baraza la Habari nchini (MCT),  John Mirenyi katika warsha ya siku moja kuhusu azimio hilo kwa wakufunzi na wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Arusha (AJTC).



wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Arusha, wakisoma maswali ya tathmini ya warsha hiyo , picha na seif mangwangi wa tanzaniasasablog

Mirenyi amesema taaluma ya habari imekuwa ikipokea waandishi wengi kila siku jambo ambalo limekuwa likisababisha baadhi yao kuvunja maadili ya uandishi wa habari na kuifanya kutoheshimiwa na jamii.

Amesema azimio la  Dar es salaam kwa wahariri , waandishi na wamiliki wa vyombo vya habari (DEFIR) limetoa mwongozo wa namna ambavyo waandishi wa habari wanatakiwa kufanya shughuli zao ili kuijengea hadhi taaluma hiyo mbele ya jamii na kuifanya kuheshimika kama zilivyo taaluma zingine.


Mwandishi Mkongwe na Rais wa chama cha waandishi wa habari za mazingira JET Christom Rweyemam akitoa mada kuhusu azimio la wahariri jijini Dar es salaam (DEFIR) katika semina hiyo

Mwandishi Mkongwe na Rais wa chama cha waandishi wa habari za mazingira JET Christom Rweyemam akitoa mada kuhusu azimio la wahariri jijini Dar es salaam (DEFIR) katika semina hiyo

Wakisikiliza kwa makini

John Mirenyi Meneja utafiti na machapisho wa Baraza la Habari Tanzania (MCT0, akimtambulisha mmoja wa waandaaji wa semina hiyo ambae pia ni mwanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Arusha

Wakimsikiliza kwa makini mtoa mada

Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Arusha AIJTC wakimsikiliza kwa makini mtoa mada (hayupo pichani).

Wakufunzi na wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Arusha, wakisoma maswali ya tathmini ya warsha hiyo , picha na seif mangwangi wa tanzaniasasablog

Mhariri wa Radio Safina  Lucas Daniel  akisaini azimio la DEFIR

No comments: