Sunday, July 21, 2013

MORANI ANUSURIKA KUCHAPWA MBOKO 7O, NI BAADA YA KUKIRI KUWACHAFUA WAZEE WA KIMILA 'MALAIGWANAN' KWENYE MITANDAO YA KIJAMII


Na Mwandishi Wetu, Tanzaniasasa
ARUSHA

KIJANA mmoja wa jamii ya kimasai Lomayani Mitewasi juzi alinusurika  kupewa adhabu ya kuchapwa viboko 70 aliyokuwa apewe na viongozi wa jamii  hiyo baada ya kutuhumiwa kusambaza taarifa  ya uongo kwenye  mitandao ya kijamii.

Adhabu nyingine aliyokuwa apewe kijana huyo ambaye ni mkazi wa kata ya Elerai  ni pamoja na kulipa ng’ombe dume  kwa kosa la kukiuka mila za kimasai kwa kutoa taarifa za uongo

Mwenyekiti wa MAA akizungumza katika kikao hicho
Kufuatia hali hiyo Mitewasi alilazimika kusimama mbele ya wazee hao wa kimila(Malaigwanani) ikwa ni pamoja na kukiri kuwa taarifa hizo ni za uongo na kwamba amekiuka mila za jamii hiyo kwa kuandika taarifa za ungo katika mitandao ya kijamii

“Wazee wangu naomba mnisamehe nilighafilika ninakiri  kuandika habari za uongo katika mitandao hiyo mimi binafsi sikijui kimasi huwa nina sikia neo mojamoja tuu japo nilikuwepo kwenye mkutano uliopita sikujua hata mlizungumza nini kwa kuwa mlikuwa mnazungumza kilugha”

Kwa mujibu wa kijana huyo mbele ya malaigwanani alisema kuwa aliandika kuwa malaigwanani wagawanyika katika makundi mawili moja linatetea CCM na Lingine CHADEMA jambo ambalo ni uongo

Pia aliandika Naibu waziri wa Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Goodluck Ole Medeye amewatumia malaigwanani kuvuruga uchaguzi mdogo wa Arusha

Mitewasi pia aliandika kuwa kikao hicho kililenga kubagua wakazi wa Arusha kwa tofauti za makabila yao, alilazimika kufuta kauli yake hiyo na kuomba radhi mbele ya Malaigwanan hao kwa kile alichodai alighafilika

Awali akitoa taarifa kwa waandishi wa habari jana, Katibu wa Baraza la MAA, Amani Lukumay alisema kuwa wazee hao wamesikitishwa sana na taarifa hizo za uongo  ambazo zilisambazwa katika mitandao ya kijamii ambayo ina lengo la kuvuruga amani ya jiji la Arusha lakini pia kuwagawanya wazee hao

Lukumay alisema kuwa lengo la kukutana kwa wazee hao wiki iliyopita ililikuwa na lengo la kuzungumzia amani ya katika mkoa wa Arusha na kwamba hakuna kitu kingine lichozngumzwa katika kikao hicho

“Onyo hili halilengi chama chochote cha siasa, bali tunavionya vyama vyote vinavyofanya shughuli za kisiasa Arusha kwa sababu Malaigwanan hatufungamani na itikadi za vyama kwani miongoni mwetu wamo wanachama wa vyama tofauti vya kisiasa,” alisema Amani.

Katibu huyo alilazimika kutoa ufafanuzi huo baada ya Malaigwanan hao waliokutana kwenye kikao cha Julai 12, mwaka huu katika eneo lao maalum ya ibada za jadi lililoko ndani ya   Chuo cha Ufundi Arusha(ATC), kudaiwa kutoa kauli zenye muelekeo wa kisiasa unaolenga kukinufaisha CCM dhidi ya Chadema.

Wakati huo huo wazee hao waliwataka waandishi wa habari kuzingatia maadili ya kazi yao kutokana na baadhi ya magazeti kuandika taarifa za uongo juu ya kikao cha mila.

waliwataka walioandika taarifa hizo kukanusha ili kuuhabarisha umma ukweli wa kilichozungumzwa na kuitoa  doa jamii hiyo dhidi ya jamii zingine kama ilivyoripotiwa katika vyombo hivyo.

No comments: