Friday, September 27, 2013

WAANDISHI WA HABARI ZAIDI YA 40 KUTOKA NCHI ZA KENYA, UGANDA NA TANZANIA WALIOKUWA WAKIHUDHURIA KONGAMANO LA MESHA NCHINI KENYA WANUSURIKA KATIKA AJALI YA MOTO BAADA YA HOTELI WALIYOFIKIA KUUNGUA

Mmiliki wa mtandao huu, Seif Mangwangi kulia akiwa na mwandishi wa habari wa Raia Mwema Paul Sarwat nje ya jengo la hoteli ya Galexon jijini Nairobi muda mfupi baada ya kukimbia ndani ya vyumba kufuatia jengo hilo kuanza kuwaka moto, hata hivyo kampuni ya ulinzi ya G4S ya jijini Nairobi ilifika baada ya zaidi ya saa moja kupita tangu moto huo ulipoanza kuwaka na kufanikiwa kuzima moto huo

Wafanyakazi wa kampuni ya ulinzi ya G4S wakijiandaa kuanza kuzima moto uliokuwa ukiunguza hoteli ya Galexon jijini Nairobi usiku wa kuamkia leo 

Katibu Mkuu wa chama cha waandishi wa habari za Sayansi, Kilimo, Afya na mazingira nchini Kenya, Aghan Daniel katikakati(mwenye shati jeupe),  akizungumza na waandishi wa habari walionusurika katika ajali ya hoteli ya Galexon kuungua moto jijini Nairobi usiku wa kuamkia leo. waandishi hao walihamishiwa hoteli ya Delta iliyoko katikati ya jiji la Nairobi

No comments: