Tuesday, November 26, 2013

biashara ya mafuta ya alizeti yashamiri stendi ya mabasi singida

Wafanyabiashara ndogondogo wa mafuta ya alizeti washamiri stendi ya mabasi singida. Hapa wakionekaba wakiuza mafita kwa abiria wa basi la igembe nsabo kama walivyonaswa na mpiga pivha wetu leo


Sunday, November 24, 2013

TMF YAKUTANISHA WAANDISHI WATEULE WA KUFANYA HABARI ZA UCHUNGUZI DODOMA HOTEL






Mhariri wa gazeti la jamboleo Ebenezer mende akizungumza na mmoja wa washiriki wa mafunzo ya waandishi wa habari za uchunguzi yanayotaiiwa kuanza hivi karibuni

Thursday, November 21, 2013

RC Arusha aagiza OCD kumtia mbaroni diwani kata ya olasiti

Mkuu wa mkoa wa arusha magesa mulongo akitoa agizo kwa mkuu wa wilaya akhakikishe diwani wa kata ya olasiti ismail katamboi anakamatwa kwa kuzuia mradi wa maji usipite ktk kata yake

Mkurugenzi wa kampuni ya ujenzi ya vest construction ltd samwel Lugemalila akimweleza mkuu wa mkoa maendeleo ya mradi huo wa maji wa km15 na changamoto ambazo amekuwa akikabiliana nazo

Fundi mkuu wa mradi wa maji paul tahiya kulia akieleza namna alivyopigwa na diwani katamboi na kupelekwa polisi, wa kwanza kushoto ni mkurugenzi wa kampuni inayojenga bomba hilo ya vest co.ltd samweli lugemalila

Sehemu ya mtaro unaotarajiwa kurandazwa mabomba kupeleka maji kijiji cha lukudivinyi kisongo wilayani arumeru

Tuesday, November 19, 2013

NYALANDU AJITOSA KUINUA VIPAJI VYA WANARIADHA SINGIDA, PIA NI KWAAJILI YA KUHAMASISHA KUPINGA UJANGILI

wanariadha wakiwa njiani kuelekea kumalizia mbio hizo 

Mkurugenzi wa Afrika Wildlife Fund, Pratik Patel akagana na mshindi wa kwanza katika mbio za nusu marathoni Paul Itambo baada ya kumkabidhi zawadi zake 

Mwanariadha, Fabiola William akimalizia mbio za Nusu Marathoni za Singida Marathoni na kuibuka mshindi wa kwanza kwa upande wa wanawake na kujinyakulia kitita cha Tsh300,000 na medali. mbio hizo ziliandaliwa na Naibu waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu kwa lengo la kunyanyua vipaji vya vijana sanjari na kupambana na ujangili wa Tembo (PICHA NA SEIF MANGWANGI)






























                                                                                                                                                             
Mshindi wa kwanza katika mashindano hayo Paul Itambo akimaliza mbio za km21 
                                                                                                                                                                                                                          
Mmoja wa washiriki wa mbio za Singida Nusu Marathoni Philemon Tengu akikimbia bila kuwa na vifaa maalum vya kukimbilia ikiwemo viatu jana katika mbio hizo zilizoanzia katika kijiji cha mitula darajani na kumalizikia katika viwanja vya shule ya msingi Ntunduu. Mbio hizo ziliandaliwa na Naibu waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyaladu zikiwa na lengo la kukuza vipaji vya wanariadha vijana na kupambana na ujangili wa tembo. (PICHA NA SEIF MANGWANGI) 



  



 NA SEIF MANGWANGI, SINGIDA
 
ZAIDI ya wakimbiaji 400 kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Singida juzi walishiriki mbio za kwanza za nusu marathoni Mkoani humo zikiwa na lengo kuu l

a kunyanyua vipaji vya wakimbiaji vijana sanjari na kuhamasisha vijana kwenye mapambano dhidi ya ujangili wa tembo nchini.
 
Katika mbio hizo zilizoandaliwa na Naibu waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu kwa upande wa wanaume,  mkimbiaji, Paul Itambo aliibuka kidedea kwa kukimbia kwa saa 1:10 na kuzawadiwa fedha Taslimu Tsh300,000, huku kwa upande wa wanawake Fabiola William aliishinda kwa kutumia saa1:53 na kuzawadiwa Tsh300,000.
 
Mbio hizo zilizoanzia katika kijiji cha Mitula Darajani na kuishia katika shule ya msingi Ntunduu, Singida Vijijini, Samuel Ikungi aliibuka mshindi wa tatu katika mashindano hayo na Emmanuel Samson alishinda nafasi ya tatu huku kwa upande wa wanawake, Winfrida Hassan aliibuka kidedea katika  nafasi ya pili na Zakhia Abdallah alishika nafasi ya tatu.
 
Kwa upande wa wanaume, mbio za kilometa tano Gabriel Galado aliibuka mshindi,  akifuatiwa na Deo Lazaro nafasi ya pili na Jonas John aliibuka nafasi ya tatu huku kwa wanawake Neema Kisunda aliibuka mshindi katika mbio hizo za kilometa tano akifuatiwa na Pascalia Sylvester.
 
Katika mbio za kilometa mbili na nusu upande wa wanawake, Julitha Anthony aliibuka mshindi akifuatiwa na Editha Gabriel na Margret Benado, huku upande wa wanaume Petro Pascal aliibuka mshindi akifuatiwa na Baraka Sebastian nafasi ya pili na Haji Swalehe alishika nafasi ya tatu.
 
Akizungumza kwa Niabu ya Naibu Waziri, Nyalandu, Mkurugenzi wa shirika la Afrika Wildlife Trust(AWT), ambae ni mwanzilishi wa matembezi ya kupinga ujangili wa tembo nchini katika matembezi aliyoyafanya kutoka Arusha hadi Dar es salaam, Pratic Patel aliwataka wazazi kuhamasisha vijana kushiriki kwenye mchezo wa riadha ili kuitagnaza Tanzania.
 
Pratik alisema Mkoa wa Singida umekuwa kinara wa mbio mbalimbli nchini hivyo ni wakati wa wazazi na wadau mbalimbali kuwekeza katika mchezo huo mkoani humo ili waweze kushiriki michuano mikubwa duniani na kuitangaza Tanzania kwa kuleta ushindi katika mbio watakazo shiriki.
 
“Riadha ni mchezo ambao utawapatia ajira vijana wengi hasa hapa Singida, ni wakati sasa kwa wazazi na wafadhili wengine kote nchini kujitokeza kudhamini riadha ili vijana watakaopatikana waweze kushiriki michuano mikubwa ulaya na kuiletea sifa Tanzania,”alisema.
 
Pratik alisema Tanzania imekuwa katika tishio la kupotea kwa wanyamapori maarufu ikiwemo Tembo hivyo vijana wanapaswa kuwa mabalozi wazuri wa kupingana na ujangili huo kwa kuwataja watu wanaohusika ili vyombo vya sheria viweze kuwachukulia hatua za kisheria.
Ends…

Monday, November 18, 2013

WABUNGE EALA WAMPONGEZA RAIS KIKWETE KUHUSU JUMUIYA HIYO

Waandishi wa habari wakiwasikiliza wabunge wa bunge la afrika mashariki walipokuwa wakimpongeza rais kikwete kwa msimamo alioonyesha kuhusu jumuiya hiyo

Kushoto katibu wa wabunge wa Eala shyrose bhanji kushoto na mbunge mwenzake adam kimbisa wakizungumza na waandishi wa habari

MAHAKAMA ZA KIMATAIFA ZATAKIWA KUSHITAKI WAHALIFU MAHAKAMA YA AFRIKA

Na seif mangwangi, AICC, ARUSHA

MAHAKAMA za mataifa mbalimbali barani afrika  zimeshauriwa  kushirikiana na mahakama ya haki za binadamu barani afrika (AFCHPR)  yenye makao yake jijini Arusha,  kutafisiri na kuelewa ulinzi wa   haki za binadamu ambazo zimekuwa zikikiukwa katika mataifa mbalimbali.. 

Rai hiyo imetolewa leo na waziri mkuu, mizengo Pinda,,alipokuwa akifungua kongamano la kwanzala majaji  linalojadili kuwepo msingi imara wa kuteteanakulinda  la  haki za binadamu kutokana na ukiukwajiunaofanywa katika mataifa mbalimbali. 

Amesema kuwa kongamano hilolinaloshirikisha majaji ambao ni wakuu wa vyombo vya kutoa haki ndani ya nchi, mahakamaza kikanda ,mahakama ya afrika  na nje kuangaliajinsi wanavyoweza kushirikiana pamoja katika kuangalia swala zima la ulinzi nautetezi wa haki za binadamu.

 Pinda, amesema kuwa Tanzania iko msitari wa mbelekutekeleza na kulinda haki za binadamu na imeridhia mikata mbalimbali naitifaki(Protocal) mbalimbali ili kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa .

Amesema kuwa eneo ambalo halijapea  nafasi kubwa  ni wakati gain kunakuwepo na ukiukwaji  wa haki za binadamu ,mashirika au mtu mmoja mmoja  anaenda mahakamani kudai haki hizo  pindi zinapokiukwa.

Pinda amesema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi 7 zilizoridhia kulindwa kwa haki za binadamu kati ya 26 barani afrika zilizosainimkataba wa kuanzishwa kwa mahakama ya afrika ambayo imetoa uhuru kwa mshirika yasiyokuwa ya kiserikali  kwenda mahakamani kudai  haki pale zinapokwa . 

Kwa upande wake Jaji mkuu Mohamed Othman  Chande, amesema kuwa kongamano hilo ni la kwanza  tangia kuanzishwa kwa mahakama ya afrika.

alisema katika kongamano hilo majaji mbalimbali majaji wamekutanishwa ikiwemo wa mahakama za kikanda na mahakama ya afrika na za kimataifa  na kwamba msingi mkubwa ukiwa ni kujadili namna ya majaji wanavyoweza kushirikiana  kutafisiri masharti ya haki za bindamu. 

Jaji, Chande amesema haki za binadamu zimekuwa zikilindwa katika katiba za mataifa mbalimbali  na kila mahakama ya nchi husika imekuwa ikizitafisiri  haki za binadamu kulingana na mazingira yake .

Amesema kuwa  kuna maamuzi ya kikanda kwa kila nchi , kimataifa ,ambapo kila mtu ana haki ya kuishi na haki hiyo ipo katika mikataba ambayo imeridhiwa na nchi 26 barani afrika ambapo Tanzania katika kutekeleza hilo imekubali mtu yeyote, kikundi chochote kwenda mahakamani kudai haki za binadamu pindi zikikiukwa.

 Awali rais wa mahakama ya afrika, Sophia Akufo, amesema ni lazima haki za jamii na watoto zilindwe.

Akasisitiza  kuwa ni muhimu kuzingatiwa kwa haki za binadamu na katiba za mataifa mbalimbali na zilindwe ili kudumisha utawala bora na wa kidemokrasia unaozingatia  sheria 

Amesema kuwa kongamano hilo linatoa mwelekeo na mtizamo  wa siku zijazo wa kuboresha utawala wa sheria na demokrasia ,uchumi na siasa nzuri zinazolinda haki za binadamu kulingana na mikataba na maazimio na matamko mbalimbali ya kimataifa kuhusu haki za binadamu.

Friday, November 15, 2013

MASHINDANO YA ARUSHA GOLF OPEN CHINI YA UDHAMINI WA LODHIA GROUP OF COMPANY YAMALIZIKA

Mwenyekiti wa arusha golf mustafali kushoto akimkabidhi zawadi mwenyekiti arusha gymkhana dkt freezby baada ya kuibuka mmoja wa washindi kwenye mashindano ya arusha open

Mwenykiti wa kampuni za Lodhia Harun Lodhia katikati akiwa na Mwenyekiti wa Golf Arusha Mustafali kushoto katika michuano hyo iliyomalizika hivi karibuni Arusha 

Harun Lodhia akipiga mpira katika mashindano hayo 

Harun Lodhia akiingiza mpira kwenye shimo

Mwenyekiti wa kampuni za Lodhia, Harun Lodhia akipiga mpira wa Golf kuingiza ndani ya shimo katika mashindano hayo ambayo aliibuka mshindi wa nne 


Mwenyekiti wa Golf Arusha Mustafal akizungumza wakati wa kufunga mashindano hayo na kutaja washindi



Mwenyekiti wa kampuni za Lodhia duniani, na mdhamini wa mashindano ya Golf Open Arusha 2013, Harun Lodhia akizungumza kabla ya kumkabidhi mshindi wa kwanza zawadi yake katika mashindano hayo yaliyofanyika viwanja vya Gymkhan Arusha 

Mwenyekiti wa Kampuni za Lodhia duniani, Harun Lodhia akimkabidhi mshindi wa kwanza ambae pia ni mwenyekiti wa GOlf Arusha Mustafali Kikombe

Mwenyekiti wa Makampuni ya Lodhia Harun Lodhia akimkabidhi Mwenyekiti wa Golf Arusha Mustafal zawadi ya mshindi wa kwanza katika mashindano hayo 

Mwenyekiti wa GOLF Arusha Mustafal akifurahia zawadi ya seti ya televisheni aina ya Sumsung kwa kuibuka mshindi katika mashindano hayo

Jimmy akipokea zawadi kutoka kwa JATN

NA SEIF MANGWANGI, GHMKHANA ARUSHA

MASHINDANO ya wazi ya mchezo wa Gofu kanda ya Arusha (Arusha Open Golf), yamemalizika jana jijini hapa kwa mchezaji Muzaffar Yusufali kuibuka mshindi wa kwanza wa jumla kati ya wachezaji 78 waliojitokeza kwenye mashindano hayo yaliyokuwa yakifanyika katika viwanja vya Gykhana jijini hapa.

Katika mashindano hayo yaliyofanyika kwa siku mbili na kudhaminiwa na  kampuni ya Lodhia (Lodhia Group of Campanies), Muzaffar alizawadiwa seti ya luninga aina ya Sumsang nchi32, nafasi ya pili ilishikwa na Francis Julius na kuzawadiwa jiko la kupikia, na nafasi ya tatu ilishikwa na Piniel Uliwa na kuzawadiwa seti ya Radio.

Nafasi ya nne ilishikiliwa na Mwenyekiti wa makampuni ya Lodhia (Lodhia Group of Campanies), ambae pia ni mdhamini wa mashindano hayo, Haroun Lodhia na kukabidhiwa Microwave, lakini hata hivyo zawadi hiyo aliitoa kwa mshindi wa tano kutoka timu ya TPC, Frank Roman.

Kwa mujibu wa Rais wa Gold Tanzania, Paul Matinez, Jimmy Mollel aliibuka kidedea kwenye kundi la washindi waliocheza bila kutoa (Gross winner) aliyezawadiwa seti ya radio , akifuatiwa na Issack Wanyeche
aliyezawadiwa Microwave.

“Mshindi kundi la wanawake (Lady Winner), alikuwa ni Madina Iddi aliyepewa Dish, na mshindi kundi la vijana wadogo(Junior) aliibuka James Samweli wa timu ya TPC Moshi na kuzawadiwa Dish, huku kundi la
wachezaji wakongwe (Senior winner), aliibuka kidedea Harbar Janshadar ambae pia alizawadiwa Dish,”alisema Martinez.

 Akizungumzia mashindano hayo Matinez ambae pia ni diwani wa kata ya Moshono, alisema mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka yalikuwa yafanyike Aprili mwaka huu lakini kutokana na ukosefu wa udhamini yalishindwa kufanyika.

Alisema baada ya kuona hivyo, walimtafuta mdhamini kampuni ya Lodhia kwa kushirikiana na kampuni ya  kimataifa ya usanifu wa madini  ya Diamond International yenye ofisi zake jijini hapa kwa pamoja
walikubali kutoa ufadhili wao.

Kwa upande wake mdhamini wa mashindano hayo Mwenyekiti wa makampuni ya Lodhia, Haroun Lodhia alisema kampuni yake kwa kushirikiana na Diamond International imeamua kusaidia mchezo wa Golf nchini ili kusaidia na Serikali kuutangaza mchezo huo kimataifa.