Tuesday, December 17, 2013

MWEKEZAJI MZAWA AANZISHA HIFADHI MPYA NCHINI, NI YA WANYAMA ADIMU KAMA FARU WEUPE

Bonde la Laroi litakalotumika kwa ajili ya uhifadhi wa Faru weupe na wanyama wengine adimu waliopotea nchini ambapo kampuni ya uwekezaji ya HUGO itawaingia kutoka nchi za nje ikiwemo Afrika Kusini na Botswana

waandishi wa habari wakimhoji mjumbe wa Serikali ya kijiji cha Laroi Kitesho Kaya kuhusu makubaliano iliyofikiana kati ya Serikali ya kijiji hicho na Kampuni ya Hugo Investment 

waandishi wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Serikali ya kijiji cha Laroi 

Mkurugenzi wa Tanzaniasasa semmy kiondo wa kwanza kulia, David Rwenyagira aliyevaa tisheti nyeupe na Claud Gwandu wa kwanza kushoto wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Serikali ya kijiji cha Laroi pembezoni mwa hifadhi ya bonde la Laroi

Mwandishi wa habari Mkongwe, Claud Gwandu (kushoto) akiandika jambo, wengine kutoka kulia kwenda kushoto ni Semmy Kiondo, Mjumbe wa serikali ya kijiji cha Laroi Kitesho Kaya na aliyevaa shati jeupe ni Seif Mangwangi 

moja ya madarasa yatakayohamishwa 

moja ya darasa shule ya msingi Olemedeye  litakalohamishwa katika eneo la hifadhi ya bonde Laroi ambapo kampuni ya uwekezaji ya Hugo imeahidi kujenga majengo mengine mapya 

Waandishi wa habari katika picha ya pamoja, kutoka kushoto ni David Rwenyagira, Claud Gwandu, John Mhala, Shaban Mdoe, Semmy Kiondo na Raymond Nyamwihula wakiwa katika picha ya pamoja mbele ya bonde la laroi litakalotumika kwa ajili ya uhifadhi wa wanyama adimu ikiwemo Faru

Mwandishi wa habari wa Sahara Media, Raymond Nyamwihula akiruka juu kwa furaha baada ya kuona bonde la LAROI litakalotumika kwa ajili ya uhifadhi wa Faru weupe na wanyama wengine adimu nchini

waandishi wa habari waliofika katika bonde la Laroi katika kata ya Mateves wilaya ya Arumeru litakalotumika kwa ajili ya uhifadhi wa Faru Weupe na wanyama adimu kutoka kushoto ni Claud Gwandu, Seif Mangwangi, John Mhala, Shaban Mdoe, Semmy Kiondo na Raymond Nyamwihula

Waandishi wa habari waliojumuika katika ziara ya kutembele bonde la Laroi litakalotumika kwa hifadhi ya wanyama adimu ikiwemo Faru weupe wakipata mlo wa mchana 

Waandishi wa habari waliofanya ziara ya kutembelea eneo la hifadhi katika bonde la Laroi wakipata mlo wa mchana, kutoka kushoto ni Semmy Kiondo( mmoja wa wamiliki wa blogu hii), John Mhala, Claud Gwandu na Shaban Mdoe


No comments: