Friday, October 4, 2013

SERIKALI YAFANYA MAAMUZI MAGUMU, YAAMURU MAJANGILI KUUWAWA WANAPOKAMATWA

NA SEIF MANGWANGI

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamisi Kagasheki amewaagiza Askari wa  wanyamapori na vikosi vyote vinavyolinda wanyama pori katika hifadhi  za Taifa na Mapori ya Akiba kuwaua majangili pindi watakapowakamata  ili kukomesha tatizo hilo nchini na duniani.

Akizungumza kwenye kilele cha matembezi ya kupinga mauaji ya tembo  duniani katika maazimisho yaliyofanyika jijini Arusha kitaifa, Kagasheki alisema kwa kauli yake hiyo anatarajia kupingwa vikali na
watetezi wa haki za binaadam lakini hiyo ndio hali halisi.
Vijana wakiwa kwenye matembezi ya kulaani kuuawa kwa wanyamapori ikiwemo Tembo, matembezi yaliyoanzia katika eneo la ofisi za TANAPA

Matembezi yakiendelea huku nyimbo mbalimbali zikiimbwa

Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Allan Kijazi akijadiliana jambo na mmoja ya waliokuwepo kwenye maandamano hayo

Mkurugenzi wa TANAPA Allan Kijazi wa kwanza kulia akinywa maji huku akirufahi jambo wakati watoto wakionyesha shoo katika maonyesho hayo

Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamisi Kagasheki akipokea zawadi kutoka kwa wanafunzi wa Upendo Academy ya jijini Arusha

Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamisi Kagasheki akihutubia mamia ya wakazi wa Arusha waliojitokeza kwenye matembezi hayo
Wanafunzi wa kituo cha kulelea watoto cha Watoto Foundation wakiwa katika picha ya pamoja na waziri wa Maliasili na Utalii Khamisi Kagasheki

“Ukiniuliza mimi nini cha kuwafanya majangili wanaoteketeza  wanyamapori wetu nitakujibu kuwa wanapaswa kuuwawa huko huko wanapokamatwa na hii itasaidia kutokomeza kabisa jambo hili ambalo
linamaliza wanyamapori wetu nchini na duniani,”alisema.

Alisema kuwa jangili yoyote akikutana na askari atakachofanya ili kujinasua ni kumuua askari huyo hivyo ni wazi kutangulia kuwaua wao itakuwa ndio suluhu ya matatizo ya kumalizika kwa wanyamapori nchini
jambo ambalo linahatarisha kumalizika kwa urithi wa Taifa la Tanzania.

 Kagasheki pia aliwageukia wanasiasa na kusema kuwa wamekuwa sehemu ya  kukwamisha jitihada za Serikali za kupambana na ujangili kwa kuwatetea  baadhi ya watu ambao wamekuwa wakihusika kuteketeza wanyamapori  nchini.

Alisema hata hivyo Serikali imelitambua hilo hivyo itapambana nao ili kuhakikisha suala la mapambano dhidi ya majangili linafanikiwa huku akiwasihi kufanya kazi ya siasa kama ambavyo wamekuwa wakiomba kwa
wapiga kura wao na kuiachia Serikali kupambana na majangili.

Kagasheki alisema ili kudhibiti ujangili nchini, Jeshi la Wanachi wa Tanzania (JWTZ), limejumuishwa kwenye mchakato wa mapambano dhidi ya majangili nchini na kuwataka majangili waliokuwepo kwenye matembezi
hayo kujiandaa katika mapambano hayo na ambao hawajakuwepo wapelekewe  salamu.

“ Najua miongoni mwetu kuna majangili napenda kuwaambia kuwa siku zenu  sasa zimefika mwisho, na wale ambao hawapo wapelekeeni salamu, Serikali kupitia kwa Rais Kikwete imeamua kuliingiza jeshi kwenye
mapambano ya kuokoa rasilimali wanyamapori na nina uhakika  tutafanikiwa,”alisema Kagasheki.

Akizungumzia sheria ambazo wamekuwa wakihukumiwa majangili, Waziri  Kagasheki alisema wizara yake inatarajia kupeleka mabadiliko ya Sheria hiyo bungeni ambayo itawezakutoa adhabu kali kwa watakaokamatwa wakifanya ujangili.

“Adhabu wanayopewa mahakamani majangili ni sawa na utani kabisa, na  ndio maana kila kukicha majangili wanaongezeka hivi sasa tumeamua kupeleka mswada wa mabadiliko ya sheria hii ili kutoa hukumu kali
zaidi na kutokomeza tatizo la majangili nchini.”alisema Kagasheki.

Awali akitoa salamu katika matembezi hayo Mwenyekiti wa Chama cha  waendesha utalii nchini (TATO), Willy Chambulo aliiomba Serikali kusitisha zoezi la uwindaji wa wanyamapori kama Tembo ili kukomesha
tatizo hilo nchini.

Pia Chambulo aliiomba Serikali kuzungumza na nchi ambazo zimekuwa  kinara wa ununuzi wa meno ya tembo ikiwemo China ili kushiriki kwenye mapambano dhidi ya mauaji ya mnyama huyo nchini na duniani.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi za wanyamapori (TANAPA), Allan Kijazi aliwataka watanzania kuungana na Serikali kwenye mapambano dhidi ya ujangili na kwamba endapo hawatafanya hivyo shirika hilo litakufa kwa kuwa litakuwa hakuna itakachokuwa ikikihifadhi.

Alisema wananchi ndio ambao wamekuwa wakikaa na majangili majumbani mwao hivyo ni wajibu wao kuwataja hadharani ili waweze kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa lengo la kunusuru maliasili ya Taifa.

Tanzania Announces Annual Tourism Award Winners



From Left to Right:  Hon. Amb. Liberata Mulamula, Tanzania Ambassador to the United States; Kent Redding, President, Africa Adventure Consultants; and Hon. Amb. Khamis Kagasheki, Tanzania Minister of Natural Resources and Tourism

David Schwenk, African Travel, Inc. accepting Tanzania Tourist Board Award at Africa Travel Association’s Presidential Forum in New York presented by Hon. Amb. Khamis Kagasheki, Tanzania Minister of Natural Resources and Tourism.

From Left to Right:  Hon. Amb. Liberata Mulamula, Tanzania Ambassador to the United States; Kent Redding, President, Africa Adventure Consultants; and Hon. Amb. Khamis Kagasheki, Tanzania Minister of Natural Resources and Tourism.



TANZANIA TOURIST BOARD ANNOUNCES
2013 ANNUAL TOURISM AWARD WINNERS
                                                                                                        
(October 1, 2013, New York, NY) Tanzania Tourist Board (TTB) announced the 2013 winners of the annual TTB Tourism awards. Hon. Amb. Khamis Kagasheki, Minister of Natural Resources and Tourism joined by Hon. Amb. Liberata Mulamula, Tanzania Ambassador to the United States presented awards to three of the honorees at the Africa Travel Association (ATA) eighth annual Presidential Forum held at New York University.  
 
The three honorees who received the TTB Award in New York were:
Elite Traveler Magazine received the Tanzania Tourist Board Luxury Travel Media Award  for extensive coverage of Tanzania including the Serengeti Migration being named as one of the top African safaris. Tova Syrowicz, Travel Editor, accepted on behalf of Elite Traveler Magazine.
African Travel, Inc. received the Tanzania Tourist Board Tour Operator Southern/ Western Circuit Award in recognition of their stand-alone safaris to the Southern/Western circuit of Tanzania which include many of Tanzania’s hidden gems such as Katavi and Ruaha National Park. David Schwenk, Sales Manager for North East, accepted on behalf of African Travel, Inc.
Africa Adventure Consultants, a Colorado-based tour operator, won the Tanzania Tourist Board Tour Operator Product Development Award in recognition of offering 34 Tanzania-only itineraries, including the “In Livingstone’s Footsteps” series; representing a 36% increase from 2012. Kent Redding, President, accepted on behalf of Africa Adventure Consultants.
The Awards program was created in 2000 to recognize and show appreciation to the travel professionals and media who have worked hard promoting and selling Tanzania in the US market, as well as to provide an incentive to increase the numbers even more in the coming years. TTB selected the Annual Africa Travel Presidential Forum to present the awards to show support for ATA’s ever expanding global reach in promoting tourism to the Continent of Africa.

 Full List of Tanzania Tourist Board Award Winners 2013
  1. Business Travel Media AwardPremier Traveler Magazine
  2. Luxury Travel Media AwardElite Traveler Magazine
  3. Tour Operator Southern/ Western Circuit AwardAfrican Travel, Inc.
  4. Tour Operator Product Development AwardInfinite Safari Adventures
  5. Tour Operator Product Development AwardAfrica Adventure Consultants
  6. Supporting  Local Airline AwardPrecision Air
  7. Hotels/Lodges/Camp Sustainable Tourism Award andBeyond
  8. Supporting International Airline AwardQatar Airways
  9. Tour Operator Humanitarian AwardAfrican Environments
  10. Tour Operator Southern/ Western Circuit AwardFoxes Safari Camps
  11. Supporting Local Charter Company AwardCoastal Aviation
  12. Lodges Tourism  Promotion AwardSerena Hotels
  13. Hotels Tourism Promotion AwardSouthern Sun Hotels
  14. Journalist AwardApolinario Tairo
  15. Blog AwardTembea Tanzania
  16. Supporting Local Media House AwardChannel 10

About Tanzania
Tanzania, the largest country in East Africa, is focused on wildlife conservation and sustainable tourism, with approximately 28% of the land protected by the Government, the largest percentage of any country in the world. It boasts 16 National Parks and 31 game reserves, 50 Game Controlled Areas, one special Conservation Area (the Ngorongoro) and three Marine Parks. It is home to the tallest mountain in Africa, the legendary Mt. Kilimanjaro; The Serengeti, home to the "Great Animal Migration" that was named the New 7th Wonder of the World by USA Today and ABC TV's Good Morning America; the world acclaimed Ngorongoro Crater, often referred to as the "Eden of Africa" and the “8th Wonder of the World”; Olduvai Gorge, the cradle of mankind:  the Selous, the world’s largest game reserve; Ruaha, now the second largest National Park in Africa; the spice islands of Zanzibar; and seven UNESCO World Heritage Sites. Most important for visitors, the Tanzanian people, with a rich history and diverse blend of cultures, are warm and friendly. Tanzania, an oasis of peace and stability with a democratically elected and stable government, celebrated its 50th Anniversary of Independence in 2011.