Thursday, April 18, 2013

SAFARI YA MWISHO YA BABU SAMBEKE KUTOKA NYUMBANI KWAKE ARUSHA KABLA YA MAZIKO HUKO KARANGA MOSHI

Ndugu , jamaa na majirani wa marehemu Babu Sambeke akibeba jeneza lililobeba mwili ya marehemu kuuingiza nyumbani kwa ajili ya ibada fupi pamoja na kutoa salamu kabla ya kuusafirisha kwenda Karanga Kilimanjaro kwa maziko, wa pili aliyevaa shati jeupe ni Mkurugenzi wa Mountmeru Millers, Arvind Mittal
watu wakitoa heshima za mwisho

Mkurugenzi wa Kibo Palace Vincent Laswai akiteta jambo na mmoja wa waombolezaji

Waombolezaji wakiwa na majonzi

Jamal akifunga jeneza lililobeba mwili wa marehemu Babu Sambeke

Jamal akifunga jeneza

Mkurugenzi wa Hoteli ya Kibo Palace Vincent Laswai akitoa neno kabla ya kupakia mwili na kuusafirisha kwenda Moshi

Waombolezaji wakiwa hawaamini kiilichotokea

Waombolezaji

Waombolezaji wakielekea kwenye magari kupanda kuelekea Moshi


Mamia ya vigogo pamoja na watu mbalimbali wafurika nyumbabi kwa marehemu Bilionea  “Babu Sambeke”Ernest Sambeke eneo la njiro jijini Arusha  kuaga mwili wake unaotarajiwa kuzikwa kesho nyumbani kwake eneo la Karanga mjini Moshi huku msiba huo ukiwa tofauti na misiba mingine iliyozoekeaka hapa Nchini

Marehemu,Sambeke alifariki hivi karibuni katika ajali ya ndege  aliyokuwa akiiendesha na pia mmiliki wa ndege hiyo ambapo ilianguka katika eneo la Kisongo na kusababisha  kifo chake Mkoani Arusha

Shughuli za kuaga mwili wa marehu zilikamilika majira ya saa 8:45 mchana huku mwili huo ukipakiwa katika gari maalumu la kifahari tayari kusafirishwa kuelekea nyumbani kwake Moshi kwaaajili ya mazishi.

Taratibu za kuaga mwili wa marehemu zilianza majira ya saa 5 asubuhi  huku wafanyabiashara wa madini pamoja wafanyabiashara wengine kutoka hapa Arusha na Moshi walionekana kutawala msiba huo
 
Katika zoezi hilo la kuaga mwili wa mareheu Padri Florentine Mallya ambaye ni mdogo wa marehemu  aliongoza misa ya kumuombea marehemu na baada ya kumaliza alitoa fursa kwa watu mbalimbali kupita mbele ya jeneza kwaajili ya kuaga mwili

Ndani ya jeneza marehemu alivalishwa nguo zake za kirubani huku ,baadhi ya wanajeshi kutoka jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) walionekana jana katika zoezi la kuuaga mwili wa marehemu ambapo baadhi yao walikuwa wamevalia sare za jeshi hilo

Hatahivyo,baadhi ya watu  walionekana katika hali ya kawaida  huku watoto wakionekana na nyuso za huzuni mda wote 

Tofauti na misiba mingine nchini watu mbalimbali walipata fursa ya kupata chakula na  vinywaji mbalimbali kwa kujihudumia vikiwemo vinywaji aina ya Bavaria ambapo watu waliohudhuria zoezi hilo walionekana wakijihudumia zaidi vinywaji vya bavaria

Magari ya kifahari yalionekana kutawala msiba huo huku barabara ya njiro ikionekana kuwa na msongamano kubwa iliyosababishwa na zoezi hilo la uwagaji wa mwili
Marehemu aliacha watoto watatu ambao ni Sia,Jamal,Getruda

No comments: