Tuesday, December 17, 2013

WAANDISHI WA HABARI WAFANYA ZIARA KIWANDA CHA NGUO A TO Z

Mtendaji Mkuu wa A TO Z Anuj Shah akijibu maswali ya waandishi wa habari waliotembelea kiwandani kwake 

baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika meza moja wakisubiri kupata chakula baada ya kumaliza ziara ya kutembelea kiwanda cha A TO Z

Msaidizi wa masuala ya utawala wa mtendaji mkuu wa kiwanda cha A TO Z Abeid George akizungumza na waandishi wa habari katika hoteli ya Texas nje kidogo ya jiji la Arusha mara baada ya waandishi hao kutembelea kiwanda cha A TO Z

Mwenyekiti wa APC Claud Gwandu (kushoto), akitoa hotuba yake kwa waandishi wa habari wa Mkoa wa Arusha katika hoteli ya Texas mara baada ya kumalizika kwa ziara ya kikazi kutembelea kiwanda cha A TO Z

Msaidizi wa mtendaji Mkuu wa kiwanda cha A TO Z George Abeid akifurahia jambo 

Wasaidizi wa Mtendaji Mkuu wa kiwanda cha A TO Z kuhusu masuala ya utawala wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa ziara ya waandishi wa habari kutembelea kiwanda hicho 


waandishi wa habari wakiwa kwenye gari kuelekea katika kiwanda cha A TO Z 

and
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika picha ya pamoja na mtendaji mkuu wa kiwanda cha A TO Z Katikati ndugu Anuj Shah aliyevaa miwani pembeni yake kushoto ni ndugu Binesh ambae pia ni Mmoja wa wakurugenzi wa kiwanda hicho 
waandishi wa habari wakiwa ndani ya Chandarua, kulia ni Angelo Mwoleka na anaefuatia katikati ni David Rwenyagira

waandishi wa habari wakitembelea kiwanda cha A TO Z wa kwanza kulia ni queen Lema, David Rwenyagira, Zulfa Mussa, Mack Nkwame na Kulwa Mayombi
NA SEIF MANGWANGI,ARUSHA

IMEELEZWA kuwa tatizo la ajira nchini litaisha endapo watanzania watabadilika na kupenda kununua bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya nchini ikiwemo nguo na kuacha kuvaa mitumba.

Hayo yameelezwa juzi na mkurugenzi mtendaji wa kiwanda  cha A to Z Anuj Shah alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wanachama wa chama cha waandishi wa habari Arusha waliotembelea kiwanda hicho.

Shah alisema Tanzania imekuwa ikikabiliwa na ukosefu wa ajira jambo ambalo limekuwa likichangiwa na watanzania wenyewe kwa kupenda kununua bidhaa za nje na hivyo kutoa ajira kwa watu wa nje.

"Ukinunua bidhaa za nje ya nchi maana yake unatoa ajira kwa watu wa nje na unakosesha watanzania wa ndani, hapa atoz tunazalisha bidhaa bora na imara na tunazisafirisha nje ya nchi na baadae mnaletewa mitumba, kama mkinunua bidhaa za ndani mtasaidia watanzania kupata ajira,"alisema Shah.

Alisema matarajio ya baadae ya kiwanda ni kuendelea kuongeza ajira zaidi kwa watanzania kutoka 8000 iliyonayo hivi sasa hadi kufikia 10,000 na kuisaidia serikali katika harakati zake zake za kutokomeza tatizo hilo.

Akizungumzia mafanikio ya kiwanda Shah alisema kiwanda hicho kinatarajia kupanuka na kuongeza wigo wa usambazaji wa bidhaa zake nje ya nchi mara baada ya viwanda vyake viwili kumalizika ujenzi wake ambapo bidhaa za zaidi ya dola bil79 zitakuwa zikiuzwa.

Hata hivyo alisema matarajio hayo yatafanikiwa endapo atapata msaada wa kutosha kutoka serikalini pamoja na watanzania kwa kuanza kununua bidhaa za ndani na kuacha kununua mitumba kutoka nje ya nchi.

"Ukiangalia nchi kama bangladesh wamekuwa wakiuza bidhaa zenye thamani ya zaidi ya dola bil70 kwa mwaka lakini ni sababu wanapata msaasa kutoka serikalini na watu binafsi, kwanini tanzania tushindwe?, tuna nguvu kazi kubwa lakini hatuitumii,"alisema.

Alisema msaada mkubwa anaotarajia kupata serikalini ni pamoja na kutathmini viwango vya bei za umeme viwandani na kuzishusha ili kuwapunguzia gharama za bidhaa wanazozalisha


No comments: