Friday, November 15, 2013

MASHINDANO YA ARUSHA GOLF OPEN CHINI YA UDHAMINI WA LODHIA GROUP OF COMPANY YAMALIZIKA

Mwenyekiti wa arusha golf mustafali kushoto akimkabidhi zawadi mwenyekiti arusha gymkhana dkt freezby baada ya kuibuka mmoja wa washindi kwenye mashindano ya arusha open

Mwenykiti wa kampuni za Lodhia Harun Lodhia katikati akiwa na Mwenyekiti wa Golf Arusha Mustafali kushoto katika michuano hyo iliyomalizika hivi karibuni Arusha 

Harun Lodhia akipiga mpira katika mashindano hayo 

Harun Lodhia akiingiza mpira kwenye shimo

Mwenyekiti wa kampuni za Lodhia, Harun Lodhia akipiga mpira wa Golf kuingiza ndani ya shimo katika mashindano hayo ambayo aliibuka mshindi wa nne 


Mwenyekiti wa Golf Arusha Mustafal akizungumza wakati wa kufunga mashindano hayo na kutaja washindi



Mwenyekiti wa kampuni za Lodhia duniani, na mdhamini wa mashindano ya Golf Open Arusha 2013, Harun Lodhia akizungumza kabla ya kumkabidhi mshindi wa kwanza zawadi yake katika mashindano hayo yaliyofanyika viwanja vya Gymkhan Arusha 

Mwenyekiti wa Kampuni za Lodhia duniani, Harun Lodhia akimkabidhi mshindi wa kwanza ambae pia ni mwenyekiti wa GOlf Arusha Mustafali Kikombe

Mwenyekiti wa Makampuni ya Lodhia Harun Lodhia akimkabidhi Mwenyekiti wa Golf Arusha Mustafal zawadi ya mshindi wa kwanza katika mashindano hayo 

Mwenyekiti wa GOLF Arusha Mustafal akifurahia zawadi ya seti ya televisheni aina ya Sumsung kwa kuibuka mshindi katika mashindano hayo

Jimmy akipokea zawadi kutoka kwa JATN

NA SEIF MANGWANGI, GHMKHANA ARUSHA

MASHINDANO ya wazi ya mchezo wa Gofu kanda ya Arusha (Arusha Open Golf), yamemalizika jana jijini hapa kwa mchezaji Muzaffar Yusufali kuibuka mshindi wa kwanza wa jumla kati ya wachezaji 78 waliojitokeza kwenye mashindano hayo yaliyokuwa yakifanyika katika viwanja vya Gykhana jijini hapa.

Katika mashindano hayo yaliyofanyika kwa siku mbili na kudhaminiwa na  kampuni ya Lodhia (Lodhia Group of Campanies), Muzaffar alizawadiwa seti ya luninga aina ya Sumsang nchi32, nafasi ya pili ilishikwa na Francis Julius na kuzawadiwa jiko la kupikia, na nafasi ya tatu ilishikwa na Piniel Uliwa na kuzawadiwa seti ya Radio.

Nafasi ya nne ilishikiliwa na Mwenyekiti wa makampuni ya Lodhia (Lodhia Group of Campanies), ambae pia ni mdhamini wa mashindano hayo, Haroun Lodhia na kukabidhiwa Microwave, lakini hata hivyo zawadi hiyo aliitoa kwa mshindi wa tano kutoka timu ya TPC, Frank Roman.

Kwa mujibu wa Rais wa Gold Tanzania, Paul Matinez, Jimmy Mollel aliibuka kidedea kwenye kundi la washindi waliocheza bila kutoa (Gross winner) aliyezawadiwa seti ya radio , akifuatiwa na Issack Wanyeche
aliyezawadiwa Microwave.

“Mshindi kundi la wanawake (Lady Winner), alikuwa ni Madina Iddi aliyepewa Dish, na mshindi kundi la vijana wadogo(Junior) aliibuka James Samweli wa timu ya TPC Moshi na kuzawadiwa Dish, huku kundi la
wachezaji wakongwe (Senior winner), aliibuka kidedea Harbar Janshadar ambae pia alizawadiwa Dish,”alisema Martinez.

 Akizungumzia mashindano hayo Matinez ambae pia ni diwani wa kata ya Moshono, alisema mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka yalikuwa yafanyike Aprili mwaka huu lakini kutokana na ukosefu wa udhamini yalishindwa kufanyika.

Alisema baada ya kuona hivyo, walimtafuta mdhamini kampuni ya Lodhia kwa kushirikiana na kampuni ya  kimataifa ya usanifu wa madini  ya Diamond International yenye ofisi zake jijini hapa kwa pamoja
walikubali kutoa ufadhili wao.

Kwa upande wake mdhamini wa mashindano hayo Mwenyekiti wa makampuni ya Lodhia, Haroun Lodhia alisema kampuni yake kwa kushirikiana na Diamond International imeamua kusaidia mchezo wa Golf nchini ili kusaidia na Serikali kuutangaza mchezo huo kimataifa.

No comments: