Saturday, August 17, 2013

NHC YAINGIA MKATABA WA UJENZI WA NYUMBA ZA WAFANYAKAZI NA HALMASHAURI YA MONDULI

NA MWANDISHI WETU, TANZANIASASA

 SHIRIKA la nyumba la Taifa (NHC), limeingia mkataba wa bilioni 5 na  Halmashauri ya wilaya ya Monduli kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za  wafanyakazi wa Halmashauri hiyo kwa lengo la kuwaondolea adha ya

mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo akimsikiliza mkuu wa Wilaya ya Monduli Jowika Kasunga akitoa maelezo kuhusu eneo ambalo litajengwa nyumba za wafanyakazi wa Halmashauri ya Monduli na shirika la nyumba la Taifa NHC, wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi msaidizi ujenzi wa NHC mhandisi Benedict Kilimba, kulia kwa mkuu wa Mkoa ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Monduli aliyevaa miwani ni Meneja wa NHC Arusha, James Kisarika
 ukosefu wa makazi  wafanyakazi wanaopangiwa kufanyakazi katika  halmashauri hiyo.

 Akitoa taarifa ya ujenzi wa nyumba hizo kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha  Magesa Mulongo, jana wilayani Monduli , Kaimu Mkurugenzi wa ujenzi wa  shirika la nyumba la Taifa, Mhandisi Benedict Kilimba alisema shirika  la nyumba limeshatenga shilingi bilioni  5 kwa ajili ya ujenzi huo  ambao unatarajiwa kuanza mapema Oktoba mwaka huu.

 Alisema Halmashauri ya Monduli imetenga maeneo mawili ikiwemo la ekari  1.8 na eneo lingine lenye ukubwa wa ekari tatu ambapo kwa pamoja  zitajengwa nyumba za ghorofa moja moja zitakazo kuwa na uwezo wa  kukaliwa na familia 40.

 “ Pia halmashauri imetupatia eneo lingine lenye ukubwa wa ekari 11  ambazo pia tutajenga nyumba ambazo tutaziuza kwa wananchi wa Monduli  na maeneo ya jirani na zitakazobakia tutazipangisha kwa wale
 watakaohitaji huduma hiyo,”alisema Kilimba.

 Aidha alisema shirika hilo liko kwenye mikakati ya kuanza ujenzi wa  miji mwili ya kisasa (satellite Town), jijini Arusha katika eneo la  Matevez na Usa river wilayani Arumeru ambayo itakuwa na huduma zote za
 kijamii ikiwemo soko la kisasa.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo akimsikiliza mhandisi Morgan Nyoni wa kitendo cha ubunifu wa shirika la nyumba la taifa NHC kuhusu michoro ya majengo yatakayojengwa katika Halmashauri ya Monduli

 “Shirika limeshapata maeneo mawili jijini Arusha ambayo tunatarajia  kuanza ujenzi wa miji ya kisasa ‘satelite town’, katika eneo la  Matevez shirika limeshapata eneo la ukubwa wa ekari 500 ambapo
 zitajengwa nyumba zaidi ya 7000 na katika mji wa Usa-river shirika  limepata eneo la ukubwa wa ekari 3000 na tunatarajia kujenga nyumba  zaidi ya 3000,”alisema.

 Alisema katika wilaya ya Longido, shirika hilo litajenga nyumba 58  ambapo ujenzi unatarajiwa kuanza Septemba 15 mwaka huu na kwamba  wilayani Karatu shirika hilo limepewa ekari 200.

 Akizungumzia ujenzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo alitoa  wito kwa wakazi wa miji ambapo ujenzi wa nyumba hizo unatarajiwa  kujengwa kuonyesha ushirikiano kwa shirika hilo kwa lengo la
 kufanikisha miradi hiyo kukamilika kwa wakati.

 Pia alitoa wito kwa watendaji wa Halmashauri ambazo bado hazijatenga  maeneo ya ujenzi wa nyumba za kisasa zinazojengwa na shirika hilo  kutenga maeneo hayo haraka ili kuwaondolewa wakazi wa maeneo hayo
 ikiwemo wafanyakazi usumbufu wa ukosefu wa nyumba za kupanga.

No comments: